google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

WATU WALIOCHUKULIWA KATIKA MAZINGIRA YA KUTATANISHA

MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA.                                   SUNDAY, 30th June 2013.



“Saa inakuja na sasa ipo, ambapo wafu wataisikia  sauti ya mwana wa Adamu”

2Wafalme3:4-27,”Ndipo akamtwaa mwanae wa kwanza…….” hizi ni habari za mfalme wa israeli ambae aliamua kwenda vitani  kumpiga mfalme wa Moabu, na alipoona kuwa vita inakuwa ngumu sana, akaamua kumtoa kafala mwanaye wa kiume. Hii ilikuwa agano la kale lakini hata sasa bado kuna watu ambao wakitaka ushindi huwa anatoa kafara ili apate ushindi, kafara hii inaweza kutolewa na mkuu wa nchi au yeyote atakaye ushindi. Inaweza kuwa ili kupata ushindi wa biashara, uongozi au mali.
1Wafalme 16:29-34, "Ahabu mwana wa Omrai lianza kutawala juu ya Israeli………..34’ Katika siku zake Hieli Mbetheli akajenga Yeriko, akatia misingi yake kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa kwanza na kuyaweka malango yake kwa kufiwa na mwana wake mdogo Segubu sawasawa na neno la BWANA alilonena kwa Yoshua mwana wa Nuni”

Biblia inasema, Ingawa tunaenenda kwa jinsi ya mwili lakini hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili, vita vyetu ni vya rohoni. Ndio maana hata tunapoimba sifa kwenye ulimwengu wa mwili ndivyio tunabomoa misingi ya kisheni katika ulimwengu wa roho, Ukiweza kuutawala ulimwengu wa roho unakuwa wumeutawala ulimwengu wa mwili bila kipingamizi.

 
Maombi: Naamuru ngome ya magonjwa, balaa, mikosi na ngome zote za giza amabazo zimeletwa kwenye maisha yako kwasababu ya kafala ziharibiwe katika Jina la Yesu. Na kama Yoshua alivyotangaza kwa atakaye ujenga tena Yeriko name naalaaniwe pepo yeyote atakaye jaribu kukufunga tena.

Huwezi kwenda kwenye utawala bila kuwekwa na  mamlaka ya rohoni, ama  mamalaka ya shetani au mamlaka ya kutoka kwa Mungu. Hivyo kiongozi ambaye hajatoka kwa Mungu ni lazima atakuwa ametoka kwa shetani kwasababu watoa kafara hizi wapo hata sasa.

NINI KINAWAFANYA WATU WANATOA KAFARA WAFANIKIWE.
Biblia iko wazi kabisa kuhusu watu wanaotoa watu kuwa kafala, swali kwanini wanafanikiwa? Ni muhimu kujua kuwa chakula cha mashetani ni damu, hivyo wachawi wanapotoa kafara ya watu wanamwaga damu ambayo kimsingi inawapa uhai na nguvu kwa mashetani, na mtu huyo anayetoa kafara huwa ananuiza damu hiyo kwa ajili ya kushindwa na kupata matatizo kwa mtu aliye mkusudia.

Damu ni uhai, Mwanzo 9:4, Kafara inapotolewa damu humwagika na kwasababu damu ni uhai, Damu hiyo hunena kwa jina lako na kwa ubaya ilikusudiwa kwayo.  Ukisoma Mwanzo 4:10, utagundua kuwa Habili alipouawa na ndugu yake Kaini, damu yake ilikuwa ikinenea katika ulimwengu wa roho. Vivyohivyo, damu inaponena mashetani huja na kuitimiza makusudi iliyonuiwa kwayo. Leo una matatizo kwasababu ya kafara iliyo tolewa na adui yako. Uwezi kuwa huru bila kunyamazisha kafara zote na damu zote zinazonena mabaya juu ya maisha yako.

Pale ambapo damu imemwagika ndipo madhabahu ya kifungo chako na ndipo sauti ya kifungo chako inapotokea na inaweza kuwa sehemu yeyote ama shambani, njia panda kuzimu ama mahali popote, ndio maana ajali inaweza kutokea na mtu mmoja tu ndio akapoteza maisha kwasababu yeye ndio aliyekusudiwa.

Unapoinyamazisha damu leo,wanaweza kwenda kumwaga tena damu nyingine kwa kutoa kafara na tatizo lako kuanza tena,cha msingi ni kubomoa madhabahu hiyo na kumteka nyara kuhani wa madhabahu hiyo na kumyonga kwa Jina la Yes,ukifanya hivo utakuwa umemkamata farasi na mpanda farasi na kuwatupa baharini.Kuna wengine huwa hawamwagi damu bali hupeleka mashataka kwenye vikao vyao vya kichawi.

Roho yako kulazwa usingizi na Mashetani.
Kama unavyojua mtu ni roho inayokaa ndani ya nyumba iitwayo mwili, hivyo Shetani anaweza kumwingia mtu na kuikaba roho yake, mtu wa namna hii huanza kusikia kichwa kinamuuma na baadaye anapata kujikuta amekufa au anaishi huku akiwa hawezi kufanya mipango yoyote kwasababu roho imelezwa ndani au anaweza kuonekana amechanganyikiwa ; mtu kama huyo aweza kufunguliwa kwa jina la Yesu.
3.Kuchukuliwa mzima mzima
Watu wa namna hii huitwa mzima mzima usiku,hapo yako ndiyo huitwa na kama huna Yesu lazima utaitika kwasababu roho yako haina ulinzi wa Yesu, Na unapoitwa unafungua mlango mwenyewe na kuifuata sauti na matokeo yake unapotea na unakuwa hauonekani. Ndio utasikia matangazo kwenye kwenye vyombo vya habari kuwa mtu Fulani amepotea kumbe kwasababu ya kuitwa.

Kwa njia hii shetani ametumia roho za watu. Shetani huamua kutumia wanadamu kwasababu roho za pepo ni rahisi kuangamizwa kwa Jina la Yesu, Hivyo huamua kutumia roho ya mwanadamu (superior).

Kutoa roho ndani ya mwili wa mtu na kuweka pepo.
Kwa kawaida mtu wa jinsi hii roho yake hutolewa na huingizwa ndani, na unapokuwa unaomba watu wa namna hii hawawezi kuangamia kwasababu Yesu anawapenda wanadamu, watu wa namna hii ni wengi kwelikweli. Watu wengi unawaona ni wagonjwa sana, wana matatizo sana ndani wanakuwa wamechukuliwa, watu wanamna hii unaweza kuwaombea muda mrefu na pepo lisitoke, ukiona hivyo tambua kuwa mtu huyo ambaye ni roho hayumo ndani hayumo ndani.


Watu hawa ndio ambao huombewa makanisani miaka mingi bila kufunguliwa lakini kumbe siri hii kuwa roho imetekwa haijajulikana kwao. Katika Jina la Yesu Kristo ninaamuru roho yako iwe huru. Na ufunguliwe kutoka katika udhaifu wako.

Post a Comment

0 Comments