google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

AMETUMWA KUKUCHELEWESHA

 

Bishop Dr. Josephat Gwajima

AMETUMWA KUKUCHELEWESHA

Jumapili,17.01.2021



Biblia inasema Mungu ametupa miaka sabini na wenye nguvu sana amewapa miaka themanini.Mwili wa mwanadamu unaukomo hivyo ulipotoka mbinguni umepewa maono na mission ya kukamilisha hapa duniani, your work is to complete your God given mission. Imeshaamuliwa kutoka mbinguni wewe utakuwa nani, sasa kuna watu wametumwa kukuchelewesha watakusema vibaya, watakusongasonga lakini usikate tamaa wewe songa mbele.

Upendo hauchoki huvumilia yote . Upendo haupo kwenye vitu, ni afadhali uoe au uolewe na mtu ambaye hana kitu lakini ana uhusiano mzuri na Mungu, Mungu atawabariki na utakuwasehemu ya Baraka hizo. Don’t look at material things to be a factor for you to be married to that person, it’s better to be part of the blessings.

Tatizo litakalo kufanya usishinde ni kuangalia shida yako na kujitazama mwenyewe, ukiangalia mawimbi utazama; unachopaswa kutazama ni kusudi la Mungu ndani yako.

Conviction is an inner assurance that even when your all five senses nor your mind doesn’t sense its presence but you keep on feeling that it will happen. It’s an art that no matter how many punch I received that distorted my face still the match isn’t over yet, I can WIN. If you feel the conviction do it, don’t wait. If you’re led by an inner conviction things are going to be possible. Taking a risk is not risk but not taking a risk is the greatest risk.

·         Philipians 4:12 ‘ I can do all things through Christ who strengthens me.’

·         Hesabu 14:11 ‘Kisha Mwenyezi-Mungu alimwambia Musa, “Watu hawa watanidharau mpaka lini? Na, mpaka lini wataendelea kutoniamini, hata pamoja na miujiza yote niliyotenda kati yao?’

-Ukiwasikiliza watu wenye hali halisi utafia kwenye eneo hilohilo wakati wanao sikiliza ushawishi watafika kwenye nchi ya ahadi.

Lazima ujue ukitaka kupata jambo yakupasa kupigana ili umiliki au ukipate. Kwa maana biblia inasema Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.’ Kumbe ni lazima ujue kupigana kwanza. Unaweza ukawa ni mtu lakini ukaingiziwa nia ya kishetani alafu unaitenda kazi ya shetani, mtu kama huyu anapokuja kwenye maisha yako anakuchelewesha kwenda kwenye hatima yako kwasababu amebeba nia ya shetani ndani yake. Jinsi unavyojisikia ndivyo ulivyoitiwa, shetani akijua unayo hatima kubwa lazima atume wakala wake wakucheleweshe.  Kila hatima ya mtu imepimwa.

 

·         Waefeso 5:15 ‘Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi. Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.’

·         Yohana 1:29-36 ‘Kesho yake Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazameni! Huyu ndiye Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa dhambi ya ulimwengu!  Huyu ndiye niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi kwa maana alikuwapo kabla sijazaliwa.’ Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini nimekuja nikibatiza kwa maji kusudi apate kufahamika kwa watu wa Israeli.”

 Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akish uka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake. Mimi nisingem tambua, lakini Mungu ambaye alinituma nibatize watu kwa maji ali kuwa ameniambia kwamba, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia kutoka mbinguni na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’ Mimi nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”Kesho yake, Yohana alikuwapo pale pamoja na wanafunzi wake wawili.  Alipomwona Yesu akipita, alisema, “Tazameni! Mwana-Kondoo wa Mungu!” 

Shetani hawezi kuzuia hatima yako ila anaweza kukuchelewesha; na ndio maana yatupasa sisi kuomba kwa bidii. Wapo watu ambao hatima zao zimecheleshwa na shetani, Ukisoma Biblia unamuona Mariam Magdalena alijazwa mapepo lakini hatima yake ilikuwa yeye kuja kuwa mwinjilisti wa kwanza duniani ndivyo na maisha yetu kila siku yalivyo kwamba kuna mahali muda huu tulitakiwa kuwepo na sio hapa tulipo kwasababu ya shetani na mawakala wake.

To overcome any obstacle in a physical realm must first overcome in the spiritual realm. What you sow in the spiritual realm will be reaped in the physical realm.

 


BONYEZA HAPA👇👇 KUANGALIA

IBADA NZIMA YA LEO JUMAPILI



                                                                                                            

 

Post a Comment

1 Comments