google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

USHUHUDA WA DADA FLORA ALIYEOKOLEWA NA MUNGU TOKA KWENYE AJALI MBAYA YA GARI

Naitwa Flora nimezaliwa mwaka  1992 ni mama wa mtoto mmoja aitwaye Debora mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi kumi na moja. Sikuzaliwa  nikiwa mlemavu nimezaliwa nikiwa mzima kabisa.

Mwaka 1999 nilipo kuwa na umri wa miaka nane niliumwa mguu mmoja wa kushoto  (niliparalaizi) nilikaa ndani muda mwingi sana bila kupelekwa hospitali  kwa sababu wazazi wangu walikua hawana uwezo wa kifedha wa kunipeleka mimi hosptali, nilikaa ndani zaidi ya miezi mitatu baada ya kukaa ndani miezi yote hiyo nikaja kupelekwa hosptali.

Lakini kila wakinipima hawaoni  ugonjwa unao nisumbua wakati  huo mguu wangu umepooza kutoka kwenye nyonga kwenda chini kama nikitaka kusogeza kitu na sogeza kwa mkono na wakati huo wote nilipo kuwa kitandani mguu wangu ulikua umeshaanza kuwa mfupi kwahiyo nikisema nisimame ni vidole tu ndio vinafika chini.

Nikapelekwa hospitali ya KCMC mwaka 2002 nilipo kuwa  darasa la pili nikaumwa tena mguu mwingine wa kulia na ukapooza kutoka kwenye nyonga kwenda chini kwahiyo miguu yangu yote ikapooza ikawa haifanyi kazi  ilipofika mwaka 2003 na mwaka 2004 nikaanza kuumwa mgongo, mgongo ulikua umenyooka tu kipindi hicho nilikuwa nasoma nikawa nawambia wenzangu mgongo unaniuma sana nikapelekwa hospitali lakini ugonjwa haukuonekana nikaanza tu kutumia dawa  lakini hospitalini nimeambiwa sina ugonjwa wowote unaonisumbua.

Nimekunywa sana  madawa lakini hakuna hata dawa iliyo nisaidia mwaka 2005 nilikuwa na urefu huu huu sikuweza kurefuka tena lakini tulipo kuwa tunatoka shule tulikutana na matangazo kuhusu mkutano wa injili lakini katika matangazo yale yakulia yameandikwa maneno tarajia muujiza wako baada ya kusoma nikawambia wenzangu siku ya mkutano nitakuwa kama nyie, nikawa na shauku sana moyoni mwangu, siku ya tatu kabla ya mkutano nikafunga  nikamwambia Mungu naomba uniponye ili nikutumikie maana nikiwa katika hali hii siwezi kukutumikia, nikamwambia Mungu ukiniponya nitakutumikia nanita tangaza sifa zako milele na milele.

Ilipofika siku ya mkutano tukaenda na wenzangu wakaniambia sasa unaenda na magongo au na baiskeli nikawambia twendeni na baiskeli, mkutano ulikuwa na watu wengi sana sikuweza kusogea sehemu ya mbele nilikua mbali sana wenzangu wakaniambia sasa itakuwaje utasogeaje pale mbele nikawaambia msiogope mkono wa Mungu sio mfupi  nitapokea hapa hapa nitasimama na nitaacha magongo.

Ilipofika saa kumi na mbili jioni maombezi yakaanza, mchungaji wa kwenye mkutano alikuwa anaitwa Michael Elivin alikua katoka Sweden, maombezi yalipoanza mchungaji akasema kama unaumwa shika sehemu unayoumwa na mimi nikashika miguu yangu nilipokua nimefumba macho na mchungaji akiwa anaendelea kuomba ghafla nikaona radi na mwanga mkali umepita machoni mwangu  nikasikia mwili wangu mwepesi nikanyanyuka hapo ndipo nilipo pokea muujiza wangu.

Kwenye ujana wangu watu wengi walikuwa wakiniuliza sana sasa Frola utaolewaje? Utabebaje mimba? Utatembeaje?, Mimi nikawambia nitaolewa kwa sababu Mungu alisema si vyema mtu huyu awe pekee yake. Na waliponiuliza kuhusu kuzaa nikawambia imeandikwa hapatakuwa na mtu tasa wala mwenye kuharibu mimba. Katika maombi yangu nikawa namwambia Mungu anipe mume ambaye anamjua wewe.

Mwaka 2016 Niliota ndoto kipindi nipo mbeya  tupo kwenye kagari kadogo tunaendeshwa lakini  gari kubwa likatuangukia nikaamka kutoka ndotoni  nikajiuliza nini maana ya hii ndoto ilipofika asubuhi nikawasimulia wenzangu tulioenda nao kufanya  huduma  lakini  nikawa najiuliza maswali mengi kwa nini nimeota hivi na hii ndoto inamaana gani lakini nikasema itakuwa ndoto tu, lakini ningejua nini maana ya ndoto nilioota yasingenikuta yaliyo nikuta.

Nikaota tena  ndoto  tulikua tumelala mimi na mama yangu mlezi na msaidizi wangu wa ndoa tukiwa tumelala nikaota ndoto  hatua kwa hatua matukio  yote ndani  ya ndoto, jinsi ilivyo kuwa tulikuwa barabarani tukapata ajali lakini nilipo amka nikasahau kuomba kabisa juu ya ile ndoto, tukaenda kanisani tukafunga ndoa.


Lakini moyoni mwangu nilikua sina amani kabisa yaani nikamwambia mume wangu mbona sina amani moyoni mwangu lakini mume wangu hakusema chochote zaidi ya kunitia nguvu, tulifunga ndoa ilipofika saa mbili usiku tulitakiwa  kuondoka kutoka Katesh kwenda Babati, tulipoanza safari yetu usiku ule lakini bado nilikua sina amani nikamwambia mume wangu tusiondoke usiku huu lakini kuna ndugu ambao waliokuwa wametufata kwaajili ya kuondoka nao.

Sikuwa na cha kufanya ilinibidi tu niondoke nao lakini  nilikua sina amani kabisa, safari ilianza usiku ule bado nilikua na hofu sana kabla hata hatujafika mwisho wa safari yetu tulipata ajali mbaya sana kama nilivyoota kwenye ile ndoto, ndivyo ilivyotokea maana sisi tulikuwa ndani ya gari ndogo aina ya Noah, ghafla tuka angukiwa na lori kubwa likaangukia gari yetu tukapelekwa hadi kwenye mtaro.

Nilipopata ufahamu nikajikuta nimesujudu na mkono wangu wa kulia umeingia kwenye stering na mkono wangu wa kushoto nimeulalia, nilipopata ufahamu cha kwanza nikaikumbuka ile ndoto nikasema mbona kama hiki kitu kimejirudia.Niliomba rehema sana kwa Mungu kwa sababu ya ile ndoto kwa maana nilijua Mungu alinionyesha lakini sikuomba.

Wakati naomba mume wangu akazinduka kutoka usingizini akauliza nini kimetokea, nikamwambia mume wangu tulia hapa hatakufa mtu hapa kwa jina la Yesu. Wakati huo vichwa vyetu mie na mume wangu vilikuwa karibu karibu kwahiyo akitikisa yeye kichwa ananiumiza na mie.

Wakati tukiendelea kuomba hapo dakika chache watu wakawa wameshajaa wanafanya process za kutusaidia, lakini tulikaa zaidi ya masaa sita hatujaokolewa kwa sababu gari yetu ilikuwa imekandamizwa sana.

Wale watu wa kutusaidia wakaanza kutuokoa mmoja kwa kutumia shoka, wanakata gari na shoka wakikubahatisha wanakuvuta nje. Ilipofika saa nane usiku nikamwambia mme wangu kama kuna kinafasi cha kutikisa mguu, basi tikisa ili watu huko nje wajua kuwa tuko hai. Mme wangu akanambia hawezi kabisa lakini mimi kwa ujasiri kabisa nikatikisa mguu nikashangaa mguu umekubali nikaanza kuita Yesu! Yesu!.

Watu wakauona mguu wangu wakashangaa kweli, hawakuamini kama kutakuwa na watu hai ndani ya gari, wakaleta tena shoka wakaanza kukata ili kutuokoa, wakamvuta mme wangu wakamwokoa.

Nikawa nimebaki pekee yangu, lakini cha kushangaza sana sisi tulikuwa tukiomba msaada watu wa nje walikuwa hawatusikii kabisa lakini wao wakiongea sisi tulikuwa tunawasikia.

Watu wakaendelea na jitihada za kuniokoa na mimi bahati mbaya sana mpini wa shoka ukavunjika, nilishtuka sana.Baadae walifata shoka nyingine wakakata gari wakanivuta wakanitoa.

Katika ajali ile walifariki watu saba ndugu wa mume wangu walikuwa wanne na wengine waliokuwa katika safari moja na sisi, ajali ile ilikua mbaya ilikua haistahiri mtu kupona kabisa lakini kwa mapenzi ya Mungu hadi leo tupo hai basi wote tuliokolewa walio kuwa wamekufa walipelekwa mochwari na sisi majeruhi tulipelekwa hosptali.

Tulipo rudi nyumbani nikajua yote yameisha, lakini ndugu wa mume wangu  walinyanyuka na kuanza kumsema mume  wangu ameoa freemason, amekuja kwenye familia yetu kuuwa  watu, niliumia sana.

 

ANGALIA IBAADA NZIMA YA JUMAPILI NA USHUHUDA WA DADA FLORA HAPA👇👇


 

Post a Comment

0 Comments