google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

FAIDA ZA KUMTUMIKIA MUNGU

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 25.01.2026
ASKOFU DKT JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: FAIDA ZA KUMTUMIKIA MUNGU

Kufanikiwa ni matokeo ya kupanga. Hata kutopanga ni kupanga. Yaani, kutokupanga ni kupanga kushindwa. Maisha ni matokeo ya maamuzi na hatua ambazo mtu anachagua. Kuna mambo ambayo ukikaa kimya bila kuchukua hatua yoyote, utajikuta umeshindwa na kupata matokeo mabaya.

Biblia inasema:

“Akasema, Basi sasa iondoeni miungu migeni iliyo kati yenu, mkaielekeze mioyo yenu kwa BWANA, Mungu wa Israeli. Ndipo hao watu wakamwambia Yoshua, BWANA, Mungu wetu, ndiye tutakayemtumikia; na sauti yake ndiyo tutakayoitii. Basi Yoshua akafanya agano na wale watu siku ile, akawapa amri na agizo huko Shekemu.” Yoshua 24:23–25

Kumtumikia Mungu hakumaanishi ibada ya maneno pekee, bali ni kuwatumikia watu kwa vitendo. Kumtumikia Mungu ni kuwatumikia watu. Mfano, mtu anaomba ili apate nguvu ya kuwaombea wengine. Mtumishi wa Mungu anaweza kuwa mtumishi wa serikali, mhandisi, daktari, au mfanyabiashara, ilimradi atumie nafasi yake kuwahudumia watu. Huduma hiyo humletea thawabu kutoka kwa Mungu.

Zipo faida nyingi za kumtumikia Mungu. Dunia imejaa watu waliotumia nguvu na nafasi zao kuwatumikia wengine, na historia yao imehifadhiwa kwa vizazi na vizazi. Mfano mzuri ni Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Rais wa kwanza wa Tanzania, aliyeishi kwa ajili ya watu. Hadi leo, kumbukumbu yake bado inaishi. Unapoishi kwa ajili ya watu, unaendelea kuishi katika kumbukumbu zao.

Si kila mtu mwenye maisha magumu ametenda dhambi. Wapo wanaotamani maisha bora lakini hawajapata fursa. Mtu aliye katika magumu hastahili kuongezewa mzigo, bali anahitaji kutiwa moyo na kusaidiwa ili asonge mbele. Mungu humbariki yule anayewainua wengine.

Faida za Kumtumikia Mungu

“Nanyi mtamtumikia BWANA, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako. Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza. ”Kutoka 23:25-26 

  1. Bwana atabariki chakula chako
    Unapomtumikia Mungu, anabariki chakula chako kwa kuondoa mabaya yote yaliyomo ndani yake ili kiwe salama na chenye manufaa kwa afya yako.
  2. Bwana atabariki maji yako
    Mungu huondoa kila tatizo lililomo katika maji unayokunywa na kuyafanya yawe salama kwako
  3. Bwana atakuondolea magonjwa
    Kumtumikia Mungu kunakufanya uishi chini ya ulinzi wake dhidi ya magonjwa.
  4. Hakutakuwa na kuharibika kwa mimba
    Hii inawakilisha mambo unayoanza lakini hushindwa kuyakamilisha. Unapomtumikia Mungu, hataruhusu mtu wala jambo lolote likuzuie, atakupa uwezo wa kuanza na kufika mwisho. 
  5. Hakutakuwa na utasa
    Mungu hukupa uwezo wa kuzaa mawazo, biashara, na mipango itakayokuletea ustawi na faida katika maisha yako. Ameweka ndani ya mwanadamu uwezo wa maendeleo.
6.    Ataongeza hesabu ya siku zako
Unapomtumikia Mungu, atakulinda, atakuongezea miaka ya kuishi, na kukuhifadhi katika hatari na changamoto mbalimbali. 
Unapomtumikia Mungu, atakulinda, atakuongezea miaka ya kuishi, na kukuhifadhi katika hatari na changamoto mbalimbali. 

Unaweza kumtumikia Mungu huku ukiendelea na taaluma yako. Kumtumikia Mungu hakuzuii mtu usiendelee kufanya kazi au fani yako. Biblia inatoa mifano ya watu waliokuwa na taaluma zao, lakini bado walimtumikia Mungu kwa uaminifu.

1.    KORNELIO

Kornelio alikuwa mwanajeshi, lakini pia alikuwa mtauwa na mchaji wa Mungu.

Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia; mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote…”
Matendo 10:1–5

2.    LIDIA

Lidia alikuwa mfanyabiashara wa rangi za zambarau, lakini pamoja na biashara yake, alikuwa anamcha Mungu. Hivyo, si lazima kuacha shughuli zako ili umtumikie Mungu, unaweza kufanya kazi zako huku ukiendelea kumtumikia Mungu kwa uaminifu.

3.    SHIFRA na PUA

Vivyo hivyo, wazalisha wa Waebrania walimtumikia na kumcha Mungu na hawakutii amri ya mfalme wa Misri:

Lakini wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, wasifanye kama walivyoamriwa na huyo mfalme wa Misri.kasema, Wakati mwazalishapo wanawake wa Kiebrania na kuwaona wa katika kuzaa, ikiwa ni mtoto mwanamume, basi mwueni, bali ikiwa ni mtoto mwanamke, na aishi. 17Lakini wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, wasifanye kama walivyoamriwa na huyo mfalme wa Misri, lakini wakawahifadhi hai wale wanaume. ” Kutoka 1:15–17

1.    DANIELI

Danieli alikuwa kiongozi mkubwa serikalini, lakini pia alikuwa mtumishi wa Mungu. Alikuwa makamu wa tatu wa rais, nab ado alimtumikia Mungu.

“Yuko mtu katika ufalme wako, ambaye roho ya miungu watakatifu inakaa ndani yake…”  Danieli 5:11


Hitimisho

Siri ya kuwa na nguvu ni kujizungushia watu wenye nguvu. Mtu dhaifu akijizungushia watu wenye nguvu, naye huimarika nakuonekana mwenye nguvu. Lakini mtu mwenye nguvu akijizungushia watu dhaifu, huanza kudhoofika. Akili kubwa kuliko zote ni kukubali kusikiliza hata wale usiowapenda. Sikiliza watu mbalimbali, kusanya mawazo tofauti, ndipo utakapokuwa na uwezo wa kufanya maamuzi yenye hekima.

Hekima kubwa kuliko yote ni kukubali kusikiliza Mawazo ya watu wengine, alafu unachakata yaliyo bora unayachukua na kuyafanyia kazi. Hii itakusaidia kufanya maamuzi yaliyo bora zaidi.  

Post a Comment

0 Comments