google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KUFUTA MASHITAKA YAKO

 

SOMO: KUFUTA MASHITAKA YAKO

BISHOP DR. JOSEPHAT GWAJIMA

TAREHE:  29.11.2020

Shetani siku zote ni mshitaki wa ndugu hivyo huangaika usiku na mchana kutafuta namna ya kutuangusha na kupata mamlaka juu yetu hivyo tunapokuwa tupo dhambini tayari tunakuwa chini ya mshitaki wetu ambaye ni shetani anakuwa na mamlaka ya kukufanya mgonjwa,au kufa kabla ya wakati kama vile mwenye shamba muda wowote autakao hulivuna shamba lake. Lakini tunaporudi nakuomba msamaha mbele za Mungu, kuoshwa kwa damu yake ndipo tunajiondoa chini ya mshitaki wetu maana imeandikwa ‘….Na katika torati karibu mambo yote husafishwa kwa damu na pasipo kumwaga damu hapana ondoleo..’ kwa maana hiyo tayari u msafi kabisa.

Mara nyingi mahakamani kitu kikubwa ambacho hufanya mtu kushinda kesi ni pale anapokuwa na mashaidi wengi wenye ushahidi sahihi. Kwenye biblia tunaitwa sisi ni mashaidi wa Kristo. Ukisoma kitabu cha Waebrania 12:1 Inaelezea zaidi, lakini pia inasema kuwa wamwaminio nao pia wanamashaidi wengi maana biblia inasema ‘.. tumezungukwa na mashaidi..’ hivyo shitaka lolote uletewalo hakika yake utashinda.

·        Je! Na Mungu huitaji mashaidi ?

Unapoamua kwenda rohoni nakuanza kuomba maana yake unapeleka mashitaka yako kwa hakimu lakini ushaidi wako ni yale maandiko kwamba ‘hatapatikana pooza wala kuaharibu mimba..’ , imeandikwa ‘..hakuna uganga juu ya israeli wala uchawi juu ya nyumba ya Yakobo…’, ‘utafanywa kuwa kichwa na sio mkia’ tayari umebeba ushaidi wakutosha kuweza kupewa haki yako kutoka kwa mshitaki.

 

Mungu huinua watu kutimiza kusudi maalum, wala si mti au mwamba au bahari ila ni mtu pekee ambae Mungu humvisha maono na muamko wa kupenya na kupasua milima, miamba mpaka kusudi litimie. Isaya aliulizwa na Bwana unaona nini? Maana yake lazima kuona kwanza ndipo jambo litimie.

 

Watu ambao hawajaokoka husema ‘mwenzetu ametutangulia mbele za haki’ lakini ukienda makaburini utakuta mwili upo maana yake mtu halisi ambae ni roho ndiye aliyetoka na mwili ndio uliofukiwa; ni kama vile karanga inavyotolewa kwenye ganda lake na ganda kutupwa. Maana yake ni kwamba MTU SI AKILI, SIO MWILI,BALI NI ROHO YENYE NAFSI ILIYO NDANI YA NYUMBA IITWAYO MWILI.

 

Kila mtu anamashitaka yake mwingine hana mtoto,ni mgonjwa, au huna kazi kwa kawaida hayo ndio mashitaka yako kwa maana si vile ikupasavyo kuwa. Katika maisha yako siku zote unapopata jambo au ukasikia ndani yako wito usigeuke nyuma kusikiliza watu wanasema nini; katika kufanikiwa lazima upambane vita bila kuogopa maana yoyote apiganaye kwa kusitasita huwezi kupata au kumiliki chochote. Usiogope kufa kwa maana tayari tulishakufa na kufufuka pamoja na Kristo. Siku zote unatakiwa kujua kuwa wanaokutakia mafanikio ni wachache na waliokinyume na wewe ni wengi.Hakuna kumiliki pasipo kupigana vita.

Kila mwanadamu ni matokeo ya mjumuiko wa formula mbili ambayo ya kwanza ni Muunganiko wa mbegu ya mama na baba kutengeneza mwili au nyumba yako ya nje alafu cha pili ni muunganiko wa roho yaani mtu halisi na nyumba yake ambayo ni mwili wenye sili ya udongo. Baada yakutungwa mimba miezi tisa ndipo unazaliwa lakini tu unapoingia duniani wachawi huona kila shehena na hazina au kusudi lako; sasa hazina hiyo ndiyo nyota ndio maana vita yako huaanza kuanzia ukiwa mtoto.

                Malaki 4:5 – Hapa biblia inaeleza kuwa kizazi cha watoto kupingana na baba yao ama wazazi kugeuka watoto wao kilihitaji roho ya Eliya lakini pia inaendelea kusema baadae atakuja mtu ambaye atakuwa na roho ya Eliya ambaye badae alikuwa ni Yohana Mbatizaji. Hapa biblia inaonyesha kuwa kwa kila jambo yupo mtu aliendaliwa kwa kwa kusudi maalum hata kama sehemu hiyo kwa akili za kawaida inaonyesha haiwezekani lakini ndivyo itakwavyo kuwa. Zacharia alishindwa kuamini yale malaika aliyosema maana tayari walishasoma habari ya Eliya na ndo maana kusitasita kwake kulipelekea kupata ububu.Haipaswi kusita pale Mungu anapoinua kusudi juu ya maisha yako, Mungu hapendezwi na watu wasitao.

Lakini pia kupitia kuzaliwa kwa Eliya kupitia mwili wa Yohana mbatizaji kunaeleza wazi kuwa upo uwezekano wakuzaliwa na jambo fulani ndani yako bila wewe kujua au majirani,ndugu,na marafiki kujua wewe ni nani au kusudi lako ni lipi. Ndio maana hata Yohana hakujua yeye ni nani maana alimuuliza Yesu ‘…. Je! wewe ni Eliya au Musa…?’ hii dhahiri ilimfanya Yesu ajue kuwa kwa kawaida si rahisi mtu kujua asili yake au roho yake ama kusudi lake ndipo alimjibu sawa sawa na uelewa wake kuwa ‘…vipofu wanaona,viziwi wanasikia,viwete wanatembea, na wafu wanafufuka!’.

·        1 Wathesalonike 4:16 ‘…. Kwasababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka juu pamoja na mwaliko wa parapanda……’

-Upo uwezekano wa mtu wa ndani yaani roho kulazwa huku mwili ukiwa unaonekana u mzima kabisa. Na ndio maana unakuta upo pale pale kila siku bila kujua sababu ni ipi hiyo ina maana kuwa aliyechukua control ya maisha yako ni roho nyingine si yako tena.

 

-Kwa kawaida kushindwa kwingi ndio kufanikiwa kwingi,vikwazo vingi ndio kupenya sana. Usikate tamaa hata kama pakiwa ni pagumu kupita.Biblia imedhibitisha wazi kuwa wenye kusudi kubwa ndio waliopigwa vita au kuwekewa kizuizi lakini waliopambana ndio waliopenya.

 

-Hivyo inapaswa kumuamsha mtu wako wa ndani, maana ndio mbeba maono yako,mwili wako upo kwaajili yakutimiza au kudhihirisha kweye ulimwengu unaoonekana (yaani ulimwengu wa mwili), amuru kila aliyepandwa ndani yako kuzuia usipige hatua kwenda kwenye hatima yako. Futa kila mashitak yaliyowekwa mbele yako ili usiwe mwenye haki wa kumiliki hazina zako.

Ukiwa na kitu ndani yako huwezi kujua kuwa unakitu mpaka utakapochukua hatua.


BONYEZA HAPA👇👇 KUANGALIA IBAADA NZIMA YA LEO JUMAPILI






 

 

 

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments