google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

NAMNA YA KUFIKIA HATIMA YAKO (MAOMBI YA MFUNGO DAY 2)

 

Bishop Dr. Josephat Gwajima

Somo: NAMNA YA KUFIKIA HATIMA YAKO

Alhamisi,  03.12.2020

Katika ulimwengu huu kuna viumbe vya aina mbili, visivyoonekana na vinavyoonekana. Kwahiyo sio kwasababu kitu hukioni basi hakipo, ni kama upepo unapovuma na miti kuyumba haoni upepo ila ni matokeo ya upepo. Hivyo ndivyo viumbe vya rohoni vilivyo yaani majini, mapepo, mawakala wote wa shetani walivyo, hawaonekani ila matokeo yao ndio huonekana na ndo maana unakuta mtu anapagawa mapepo au anakuwa mgonjwa. Kwahiyo ule uwezo wa wao kuona utakuwa nani baadae ndio sababu huinua vita dhidi yako bila wewe kujua kwasababu huwaoni. Tayari kwenye ulimwengu wa roho viashiria vya hatima yako huonekana na mbinguni Mungu na malaika anatengeneza njia ya wewe kufika na wakati huohuo shetani na kamati yake wanapambana usifike.

·       Warumi 8:30- ‘Na wale aliowachagua tangu asili..’ maana yake tayari tunaasili zetu tokea mbinguni kwa maana Mungu anasema ‘Maana mawazo ninayo wawazia ninyi si mabaya..’ kwahiyo anakua ameandaa mengi mazuri lakini unapokuja duniani shetani anaingia hapo kati kukuzuia  

 Luka 21:22 ‘Kwakuwa siku hizo ndizo za mapatilizo,ili yatimizwe yote yaliondikwa’ pia Luka 18:31’….na mambo yote yatatimizwa,Mwana wa adamu aliyoandikiwa na manabii’ maana yake lipo jambo ambalo kila mmoja ameandikiwa litimie.


Lakini haimaanishi kwamba umeandikiwa hayo basi unakaa na kusubiri yatimie au nabii akatabiri ukaamini bila kuweke jitihada zozote ukisoma Luka 18:31. Nabii anapokuwa anatoa unabii anazungumza ambayo Mungu amemfungulia rohoni kuhusu wewe kwahiyo anapokuambia ni jukumuu lako kuyachukua na kutendea kazi.

Ukisoma kitabu cha Isaya 11:1 na Isaya 7:1 hapo Nabii Isaya alikuwa akionyeshwa kuwa miaka ijayo Yesu atazaliwa, sasa vilevile na wachawi wanaona kuwa miaka ijayo yupo mtu atazaliwa ambaye ataharibu kazi zao. Na ndio maana unakuta waombaji wengi walipokuwa wadogo walikumbana na changamoto hatari sana au hata akiwa anakua alipitia misukosuko mingi mno Mfano, anazaliwa kabla ya wakati, anakuwa mgonjwa kwa muda mrefu au hata kukataliwa na wazazi wake.

·       Isaya 9:6- Isaya anaeleza unabii kwa kutumia wakati timilifu akisema, ‘Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanaume;na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake…’ maana yake kwenye ulimwengu wa roho tayari yaliyoandikwa kuhusu  Yesu yalikuwa yameshatimia bado tu kudhihirika ndivyo hivyo na hatima zetu zilivyo kwa bidii ya kuomba ni wakati tu kuyaona. Lakini wazuiaji wapo kama vile wana wa Israeli walivyokuwa wamepata Musa wakuwatoa Misri ila akainuka Farao na kuufanya muujiza wao kuwa mgumu kutimia ila kwa mkono wa Mungu wakashinda. Kumbe basi siri ya kudhihirika kwa hatima zetu ni kuomba kwa bidii bila kukoma.


         BONYEZA HAPA👇👇 KUANGALIA IBAADA NZIMA YA LEO ALHAMISI



 

 

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments