google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

TUMEFICHWA NA KRISTO (HATUONEKANI) (MAOMBI YA MFUNGO DAY 3)

                              

Bishop Dr. Josephat Gwajima

SOMO: TUMEFICHWA NA KRISTO (HATUONEKANI)

Ijumaa, 04.12.2020 


Wakolosai 3:1-3 ‘….kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu..’.  Kuna mambo mawili ambayo inabidi kujifunza ambayo ni kwa maana mlikufa’ na uhai wenu umefichwa’.

Silaha kubwa ya kivita ni kumuona adui hata kama unasilaha kubwa kuliko mwingine.Ukisoma Wagalatia 2:20 ‘Nimesulubiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu….’ Maana yake sisi tulikufa tayari na hatumo/hatuonekani maana tumefichwa na Kristo.

Wachawi wanapoenda nyumbani mwa mtu lazima wakuone na hawaishii kukuona tu ulivyo mwilini bali hatima yako yaani utakuwa nani, utaoa au kuolewa na nani, nani atakaezaliwa kupitia tumbo lako? kwahiyo mashetani ndio husema tu mchukue huyu mtu. Lakini tofauti ya mtu aliyeokoka na asiyeokoka nikuwa mashetani hawawezi kukuona kama umeokoka kwa maana umefichwa pamoja na Kristo. Unapookoka na kumpokea Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako tayari unakuwa umefichwa na Kristo.

·       Always remember “So as to succeed in any sphere of life you need to import spiritual facts from the bible in your life and live accordingly”; you can also refer in the Book of Galatians 2:20.


Ezra 10:14 ‘Inuka; maanca shughuli hii inakuhusu wewe; na sisi tu pamoja nawe; uwe na moyo mkuu, ukaitenda.’ Usiache kuomba na ujue siku zote shetani hawezi kukuuwa bali anauwezo wa kukujaza hofu ambayo itakusababishia mauti. Mungu ni neno kwaiyo kumshambulia Shetani tumia andiko lolote kwa maana ndio silaha yetu ya vita. Vaa ujasiri wa kumkabili shetani kwa maana ushindi tunao tayari.

Nena kwa lugha muda wa kutosha na usome maandiko kwa maana ndio njia ya kupambana na adui shetani kwa yoyote aliyeokoka. Na ndo maana ukilala ukiwa umeachia andiko ‘Mimi ni mwali ya moto’ au ‘Mimi ni chumvi ya ulimwengu’ pia ‘Mimi ni rungu na silaha za Bwana za vita’ ndivyo adui akuonavyo na ndio maana tunasema HATUONEKANI  kwa maana tumefichwa na juu yake tumepewa mamlaka ya kutamka na ikawa.

Shetani hufanya wakristo wengi waliokoka kujiona wakawaida ili aweze kuzuia kusudi la Mungu lakini wewe ambao tayari Mungu amekufunulia haya kazana kunena kwa lugha. Kuna mambo ambayo ukiwa unaomba Mungu anatengeneza connection kwenye ulimwengu wa roho.

 Lakini wakati wote inabidi kuchunga mambo matatu (3);

1. Chunga cha kuangalia

-Shetani hutumia kile ulichokitazama kuharibu nafsi yako. 

2. Kataa kusikiliza baadhi ya vitu

-Vitu unavyosikia husababisha uwepo wa Bwana kutoweka. 

3. Kataa kwenda mahali ambapo roho wa Bwana hakuruhusu

-Kama mbegu isivyoweza kumea kwa baadhi ya eneo ndivyo na roho zetu zilivyo.





BONYEZA HAPA👇👇 KUANGALIA IBAADA NZIMA YA LEO IJUMAA




 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments