google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

TUPO VITANI (MAOMBI YA MFUNGO DAY 1)

 

Bishop Dr. Josephat Gwajima

Somo: TUPO VITANI

Jumatano, 02.12.2020



Hatima za watu hazipimwi na binadamu bali Mungu mwenyewe tayari ameshapanga na kukufahamu. Lakini shetani pia anaouwezo wakufahamu umebeba nini au utakuwa nani ndio maana kuna vita ya rohoni. Tayari Mungu amepanga kuwa utakuwa nani na utafanya nini, sasa kuna watu ambao wamesheheni au wamebeba vitu vingi hivyo hata vita yao inakuwa kuwa kubwa zaidi.

   Mfano, Daudi alikuwa amesheheni vitu vingi ndo maana vita yake ilikuwa kubwa. Kwanza hakuwa mtoto anaethaminiwa na familia yake,ila pia baada ya kumpiga Goliathi bado aliibua vita na Sauli.

Uwezo wa kushinda vita yako au kuvipita vikwazo vyako ndio uwezo wako wakumiliki. Maombi ndio njia kubwa yakufungua shehena zako kwahiyo juhudi yako katika maombi

·       Luka 3:21 -Huu mstari unaonyesha tofauti ya Yesu Kristo na watu wengine waliobatizwa. Baada tu ya Yesu kubatizwa alianza kuomba na mbingu ikafunguka lakini wengine wote walibatizwa lakini mbingu hazijafunguka kwasababu hawakuomba.

Upo uwezekano wa mtu kufa kabla ya yale ambayo ameyabeba hayajatimia kama hutotia bidii. Kuna watu wanahatima kubwa ila wanaweka hofu ambayo huzuia kutimia kwa kusudi lao.

·       Yohana 21:17-Hapo Petro anaaambiwa atakuwa mzee lakini baadae Petro akaja kukamatwa kabla hajawa Mzee.Ukisoma Matendo12:1…unaeleza namna Petro alivyotaka kuuwawa kabla hata hajaandika kitabu cha Petro.Hapo tunajifunza wapo watu wanaweza kufanya hatima yako isitimie;lakini baada tu ya wale wanafunzi kuamua kuomba kwa bidii malaika akamtokea Petro gerezani na kumtoa nje.

 

Ni vyema kujifunza kuomba kwa bidii bila kukoma ukiwa umepata au umekosa kwa maana maombi hukaa akiba, maombi ambayo unaomba leo yanaweza kubadilisha maisha yako baada ya miaka mitano ukiwa hukumbuki kabisa ama huna nguvu za kuomba. ‘Kuomba kwake mwenye haki kwa faa akiomba kwa bidii..’ kazana kuomba kwa bidii sana.

Kufanikiwa katika maisha sio kuwa na utajiri bali kutimiza wito wako ulioitiwa duniani. Lile jambo linalokusukuma kila mara ufanye au linakukereketa kulitimiza ndio kusudi lako.

·       Matendo 9:19 – Hapa Paulo anaonyeshwa baada ya kuokoka alitafutwa kuuwawa ila huku aliahidiwa kuhubiri kwa mataifa mbele za wafalme lakini pia wakati huo hakuwa ameandika kitabu hata kimoja kwenye

·        2Wakorintho 11:31-33 anaeleza jinsi watu walivyoandamana kumuua hata ikabidi kushuka kwa kikapu.Ila kusimama na Mungu ndio kilichomwinua Paulo mpaka hatima yake au kusudi lake la kuhubiri,kuandika vitabu sawa sawa na neno la Bwana.

Kuna watu wanatumwa kukuharibia anaweza kuwa rafiki, mume/mke,jirani au hata wazazi ama ndugu.

Matendo 14:19 –Hapo mstari unaelezea jinsi Paulo alivyopigwa na watu ambao walipanga kumuua hata kabla neno la Mungu halijatimia au kusudi lake halijadhihirika. Unapoamua kufunga na kuomba unaharibu kila mipango ya adui zako na kukusaidia kufungua njia yako na kupita katikati yao.          

 

BONYEZA HAPA👇👇 KUANGALIA IBAADA NZIMA YA JUMATANO



 

 

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments