google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KUGEUZWA KUWA MTU MWINGINE.

 

UFUFUO NA UZIMA UBUNGO CATHEDRAL.
IBADA YA JUMAPILI 4TH JUNE 2023
ASKOFU BARAKA THOMAS TEGGE.
SOMO: KUGEUZWA KUWA MTU MWINGINE.

Vile ulivyo unaweza ukawa mtu mwingine, Mungu anapokuwa na shughuli na mtu anamkuta mtu akiwa na maisha anaona ndio yakwake kama vile amefika ila Mungu ana jambo kubwa vile ujawahi kuwaza, Mungu ana mawazo makubwa sana na anapotaka kuyatimiza hayo mawazo kupitia wewe ana desturi yakumgeuza huyu mtu na kuwa mtu yule amtakaye.

Ndipo Samweli akatwaa kichupa cha mafuta, akayamimina kichwani pake, akambusu, akasema, Je! Bwana hakukutia mafuta [uwe mkuu juu ya watu wake Israeli? Nawe utamiliki watu wa Bwana, na kuwaokoa na mikono ya adui zao; kisha hii itakuwa ishara kwako ya kuwa Bwana amekutia mafuta] uwe mkuu juu ya urithi wake. Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na wanaume wawili karibu na kaburi la Raheli, katika mpaka wa Benyamini huko Selsa; nao watakuambia, Punda hao uliokwenda kuwatafuta wameonekana; na tazama, baba yako ameacha kufikiri habari za punda, anafikiri habari zenu, akisema, Nifanye nini kwa ajili ya mwanangu? Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na kufika kwa mwaloni wa Tabori, na hapo watu watatu watakutana nawe, wanaokwea kumwendea Mungu huko Betheli, mmoja anachukua wana-mbuzi watatu, na mwingine anachukua mikate mitatu, na mwingine anachukua kiriba cha divai; nao watakusalimu na kukupa mikate miwili; nawe utaipokea mikononi mwao. Baada ya hayo utafika Gibea ya Mungu, hapo palipo na ngome ya Wafilisti; kisha itakuwa, utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakishuka kutoka mahali pa juu, wenye kinanda, na tari, na kinubi, na filimbi mbele yao, nao watakuwa wakitabiri; na roho ya Bwana itakujilia kwa nguvu, nawe utatabiri pamoja nao, nawe utageuzwa kuwa mtu mwingine. Basi, hapo ishara hizi zitakapokutukia, fanya kama uonavyo vema; kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe. Nawe utatelemka mbele yangu mpaka Gilgali; nami, angalia, nitakutelemkia huko, ili kutoa sadaka za kuteketezwa, na kuchinja sadaka za amani; siku saba utangoja, hata nitakapokujia, na kukuonyesha yatakayokupasa kuyafanya. Ikawa, alipogeuka kumwacha Samweli, Mungu akambadilisha moyo; nazo ishara zile zote zikatukia siku ile ile. Basi, walipofika Gibea, tazama, kikosi cha manabii wakakutana naye; kisha roho ya Mungu ikamjilia kwa nguvu, naye akatabiri kati yao. Ikawa, wote waliomjua zamani walipoliona jambo hilo, kwamba, tazama, huyo anatabiri pamoja na manabii, ndipo watu wakasemezana, Ni nini hilo lililompata mwana wa Kishi? Je! Sauli pia yumo miongoni mwa manabii”.1Samweli10:1-11

Hii ni Habari ambayo unaifahamu, habari ya kijana mmoja wa familia ya Benjamini alikuwa anachunga na kufuga mifugo na baba yake mzee Kishi, anakaa sehemu ambayo ni ukoo wa watu wa maskini wakawaida kabila dogo la Benjamini. Kwa hiyo huyu kijana wa kabila dogo kuna mambo hufanya watu wakaheshimika na kudhaniwa wanaweza kufanya mambo makubwa kwasababu ya kabila ambalo ametoka, hata hapa kwetu ukisema kabila lako watu wanaweza kubashiri unaweza kufanya mambo gani. Ukisema kabila lako wataweza kusema unafaa kucheza ngoma au mchawi au unaweza kufanya biashara ukisema tu kabila.

Kijana huyu alipoteza punda na kuanza kuwatafuta punda wa mzee Kishi sehemu mbalimbali wakafika mahali wakaamua waache kutafuta punda warudi nyumbani lakini mtumishi wa mzee Kishi aliyekuwa na Sauli akamwambia mji huu kuna mtumishi wa Mungu ambaye akisema neno huwa linatokea tumuende yeye. Wakaenda wakafika kwa Samweli, Samweli alipomuona Sauli, maandiko yanasema Mungu akamwambia huyu ndiye niliyekuambia mpake mafuta, maana siku moja kabla Mungu aliishamfunulia Samweli kuwa atamletea mtu ampaka mafuta ili awe mfalme wa Israel, Sauli alizania anaenda kutafuta mambo ya kimwili lakini amekutana na mtu wa Mungu ana jambo la mbinguni nakuanzia pale akabadilika akaacha kuwa mchunga punda na kuanza kutumikia kusudi la maisha yake.

Umekuja mahali hapa ili uaambiwe maneno ambayo kabila lako hawafanyagi maana utageuzwa nakuwa mtu mwingine, unaweza kusema nilikuja hapa nimelogwa, nimepoteza hata Sauli anadhania ni punda kumbe hata Mungu anaweza kubadilisha ili upate cha thamani zaidi, Mungu anaweza kufanya upoteze ndoa, masomo ili ukutane na mtu wa hatima yako.

Mungu huwa anapeleka watu kwa mtu, akitaka akubadilishe hakutokei wewe maana hutamuelewa, maisha ya watu yanabadilika wanapokutana na watu wengine wenye maelekezo ya Mungu kwa habari ya hatima yako nasio kila mtu.

Hata wewe umeletwa na Bwana, maana anataka akugeuze uwe mtu mwingine kabisa. Samweli akaambiwa ampake mafuta sauli na Roho wa Mungu akamjilia yeye kwa nguvu, kazi ya Samweli ilikuwa ni kumbaini ni nani tu na kumpaka mafuta, mengine Mungu atamaliza.

Kuna mambo watu wanayatamani ila wewe umewekewa biashaara ambayo watu wanaitamani, umewekewa ndoa ambayo watu wanaitamni umewekewa kazi ambayo watu wanaitamani. Unaweza sema mimi kabila langu mbona halina mambo hayo, hata kama ni kabila dogo maana kabila lako halina chakufanya na hatima yako maana yupo Mungu ameanda mambo ambayo watu wanatamani amekuwekea wewe. Samweli akachukua kichupa cha mafuta akamwagia kijana huyu ambaye hajawahi kuwa na ndoto yakuwa mfalme na hata yeye alienda kwa Samweli sio ana mfahamu hapana anayemfahamu Samweli ni mtumishi wa Sauli, Sauli alikuwa mbishi na kuweka vikwazo ni kama kwamba hayaki kwenda lakini ndiye aliyewekewa. Samweli alimpaka mafuta na kumwambia Bwana amekufanya kuwa mkuu juu ya Israel. Mungu kama bado hajakufanya mkuu unatakiwa usubiri na ukajikuza kuwa mkuu Mungu atakupiga maana Mungu huwapiga wajikuzao subiri wakati wa Bwana wakukufanya kuwa mkuu na kuna eneo kabisa la wewe kuwa mkuu. Kila eneo lina watu wakuu na Bwana ndio ana wafanya kuwa wakuu, akasema atawamiliki watu wa Bwana na utawaokoa na adui zako na sasa nakupatia ishara ili ujue kuwa hayo mambo yatatokea, ishara ya kwanza ukitoka hapa kwangu utafika karibia na kaburi la Raheli pale Selsa utakutana na watu wawili hao watu watakuambia punda wakwenu wamepatikana na mzee ameanza kuhofia habari yako hao achana nao utaendelea mbele mpaka kwenye Mwaloni wa Tabori, utafika kwenye Mwaloni wa Gaboni utakutana na wanaume 3, wa kwanza ana wanambuzi watatu wapili ana mikate mitatu na watatu ana kiriba cha divai, bila kuwaomba watakupa tu, mafuta hufanya kupewa vile ambavyo hujaomba, mafuta huleta mvuto watu watakuona una kibali kwao, mafuta ya Bwana yakufanye uwavutie watu kwenye biashara, kazi uwe na kibali kwa watu. Usichanganye na mafuta mengine yakukanyaga naongelea mafuta ya bwana.

Mafuta mtu akipakwa Roho wa Bwana anamjilia kwa nguvu, neno la Bwana linatosha Yesu alipokuja kuna mambo yalikoma maana alitupatia mamlaka akatuachia neno na neno la Bwana lina nguvu zaidi ya mafuta, vitambaa hata Yesu hakuwa na mafuta alikuwa na neno la Bwana, Yesu alimwambi Petro kuna baadhi ya watu wameniacha na nyie mtaniacha? Petro akamjibu tuende kwa nani mwenye neno.

Neno la Bwana ni kali linachoma ni jepesi kutambua mawazo ya mwanadamu fuata neno nenda neno lilipo sio mafuta wa chumvi hapo mwanzo palikuwa na neno sio vitamba wala chumvi palikuwa na neno na neno alikuwa kwa Mungu na neno alikuwa Mungu na vyote vilifanyika kwa huyo na pasipo yeye hakuna ambacho kilifanyika ndani yake umo uzima na uzima ni nuru nayo nuru ya ng`aa gizani wala giza haliwezi kulishinda.Wafalme watatu, Mfalme wa Israel, mfalme wa Yuda na mfalme wa Moabu wamefika mahali wamekwama hakuna maji  wakaanza kuulizana jamani hivi mji huu kweli hakuna mtu wa Mungu tumuulize, mmoja akasema kuna kijana alikuwa anamwaga maji kwenye mikono ya Eliya, akasema huyu ana neno la Bwana, kuna kosa kubwa linafanyika kukuza vitu ambavyo sio sahihi, kukuza vitambaa, mtu hana neno la Bwana ila ana stoo ya maji, na neno la Bwana likae kwa wingi, Ukristo unakuwa dhaifu kwasababu watu wanataka kunywa mafuta au kumwagiwa ila hapendi kukaa chini kusikia neno. Yesu alikuwa mwalimu hakugawa maji wala mafuta alifundisha neno na wakati mwingine pepo walitoka kwa kusikia neno tu. Hata kama una sura mbaya ila una upako basi unavutia. Hata kama anakula asali ya mwitu, anavaa nguo za singa ila anaupako basi anavutia, kijana ambaye hujaoa ila anaupako nakuambia utaoa yeyote maana watu wataacha kazi zao wakufuate wenye pesa na wasio nazo, wakubwa kwa wadogo watakufuata muone Yesu alikuwa na upako na watu wakamfuata na habari zake zikaenea kotekote na wasomi wanawake wenye mali wakamfuata nakumtumikia na mali zao. Maana anasema Roho wa Bwana yu juu yangu Bwana amenipaka mafuta, Bwana akikupaka mafuta utavutia watu wakila aina. Yohana walimfuata mpaka porini kwa sababu ya mafuta aliyopakwa.

Ishara ya tatu, Gibea ya Mungu palipo na ngome ya wafilisti utakutana na manabii wanatabiri, Roho wa Bwana atakujilia kwa nguvu nawe utakuwa mtu mwingine, kuna watu walikuwa hawafai wanaoga ila wamefika hapa wamekuwa majasiri wananena kama sisi. Maandiko yanasema akaanza kutabiri akashangaa watu, wakasema nini hiki kimempata mwana wa Kishi. maana Sauli hayumo kwa manabii wala hajasoma kozi ya kunena ila ni Roho wa Mungu amemjilia kwa nguvu. Mtu ni roho ukitaka badiliko lolote lazima lianzie rohoni na badiliko lazima liletwe na roho ukishughulika na mtu wanje unapoteza muda maana mtu ni roho, shughulika na roho, badiliko la mtu wanje sio la kudumu ni lamuda kitambo tu badiliko lianzie ndani. Sulemani anasema hata ukimpiga mpumbavu ukamtwanga kwenye kinu, bado hata badilika. Unamuona mgerasi anaishi makaburini watu wakamshika wakamfunga wanataka kumsaidia wakamfunga wakamvisha nguo walipotoka akavunja minyororo ili awakomeshe akaenda kukaa sehemu watu hawafiki kwenye makaburi ila siku mmoja Yesu wa Nazareti akaenda akamkemea maandiko yanasema baada yahapo alikuwa amekaa na Yesu na amevaa nguo na ana akili zake. Kuna mambo mtu akiyafanya sio ya akili yake, mwanadamu ana mambo ambayo sio ya akili yake na ambao niya akili yake ukiona mwanadamua anatembea uchi ujue sio akili yake kama binti anatembea maziwa yako nje kama anauza maziwa ina maana hana akili zake kuna maeneo ya mwili yako hakuna mtu anatakiwa kuyaona zaidi ya mume wako na mkiwa wawili tu.

Kubadilika ni mtu kuanzia ndani. Alipokutana na Yesu akamkemea akavaa nguo bila kuambiwa, kuna jambo Mungu anataka kufanya kupitia wewe ila haitawezekana mpaka akubadilishe, Sauli alitamkiwa maneno akabadilishwa neno la Mungu linaweza kubadilisha mtu maana neno la Mungu ni Roho tena ni uzima. Kusikia neno la Mungu tena na tena unabadilika wengine kuhubiri, biashara, nafasi fulani kazi sasa hivi ulivyo huna sifa ila utageuzwa kuwa mtu mwingine, maandiko yanasema kuna mambo jicho halijawahi kuona sikio halijawahi kusikia ameandalia wamchao. Utanzaa kufanya mambo yasiyoya asili yako watu watashangaa. Ukipuuzia mambo ya Rohoni unapuuzia hatima yako, watu wanamuda na shule, watu wengine hata mvua inyeshe vipi lazima uende shule au kazini ila kanisani wingu tu ukiona hauendi kanisani.

Bwana akanena na Musa, na kumwambia, Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda; nami nimemjaza roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina, ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba, na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.Tena, tazama, nimemchagua, awe pamoja naye, huyo Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani; nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima, ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza; yaani, hema ya kukutania na sanduku la ushuhuda, na kiti cha rehema kilicho juu yake, na vyombo vyote vya Hema; na meza, na vyombo vyake, na kinara cha taa safi pamoja na vyombo vyake vyote, na madhabahu ya kufukizia uvumba; na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake; na mavazi yenye kufumwa kwa uzuri, na mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani;”Kutoka 31:1-10

Mungu anataka mtu awe fundi ila mtu huyo sio fundi wakati huo, mtu huyo yupo jangwani wanatoka Misri kwenda Kanaani ila Mungu anataka mtu awe fundi na hakuna veta, anatakiwa atengeneze vitu ambavyo Musa ameona katika ulimwengu wa Roho bila kusimuliwa, Mungu anataka awe fundi, Mungu anakuwazia jambo ila haongei nawewe, Mungu anaongea na Musa akaongee na Bezaleli, Mungu aliongea na Samweli sio Sauli anaongea na mtu mwenye mamlaka juu yako aje aongee na wewe. Mungu anajua kutengeneza vitu zamani walikuwa wanachora kwenye magome ya mti, Roho wa Mungu atamgeuza. Kuendelea kusudi la Bwana lazima ugeuzwe huwezi kwenda na akili yako hiyo Roho atawajilia kwa nguvu, Samson hakuwa mtu wa kawaida akamwambia Delila mkininyoa nywele nitakuwa mtu wa kawaida ina maaana hakuwa wakawaida, Samson Roho wa Mungu alimjia kwanguvu akaenda akanyanyua geti na kupanda nalo mlimani. Kuna kazi Mungu anataka uifanye. Kuna jambo hapa anataka ulifahamu.

Basi, hapo ishara hizi zitakapokutukia, fanya kama uonavyo vema; kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe. Nawe utatelemka mbele yangu mpaka Gilgali; nami, angalia, nitakutelemkia huko, ili kutoa sadaka za kuteketezwa, na kuchinja sadaka za amani; siku saba utangoja, hata nitakapokujia, na kukuonyesha yatakayokupasa kuyafanya”. 1Samweli 10:7-8

 Roho atakapokujilia kwa nguvu chochote utakachoona vema fanya hapa ndipo hatima za watu zimelala, wewe ndio unaona vema sio jumuiya yako, mtu Mungu amemvuvia aanze biashara na anatoka kwenda kumuuliza mtu anakuvunja moyo, ila ulivuviwa wewe pekee yako. Ishara hizi zikitokea fanya na usipo fanya utakuwa yule yule wazamani, ukiishaona fanya usianze vikao vya kuzungumzia fanya. Mungu anamwambia Kornelio tuma watu waende kumuitia Petro maana zamani ilikuwa hairuhusiwi kwenda kwa Wayahudi ila Bwana amesema tuma watu huko huko kwa hao wasiochangamana na watu. Hatima imefichwa kwenye mambo usipofanya utabaki kuwa yule yule.

Chukua hatua kuna maelekezo ya Mungu huonekana hayaeleweki, mpaka uchukue hatua ndio utaelewa. Ibrahim kwa Imani alipoitwa akaitika kwa Imani akatoka asijue aendako. Eliya aliambiwa toka hapa nenda nimekuandalia mwanamke mjane akulishe, akaenda akafika akamkuta mwanamke akamwambia naomna maji pia njoo mkate, mwanamke akamwambia nimebakiza konzi moja ya unga na mafuta nipike nile na mwanangu ale tukafe akamwambia nitengenezee mimi kwanza na mwanamke akafanya hivyo akampikia Eliya kwanza na unga na mafuta hayakuisha mpaka siku Bwana alipoleta mvua.

Maisha ni mapigano tegemea upinzani tokea mwanzo, jiandae kutokukata tamaa mpaka ukuta uanguke. Fanya biashara fanya ufundi mafanikio yamefichwa kwenye mambo unafanya hatua kwa hatua, kidogo kwa kidogo hata kama hujui vingi utajua vingine mbele ya safari. Mungu atakuandalia mtu akufundishe biashara akufundishe kwa ustahili zaidi lakini lazima uanze anasema ameweka watu kwa ajili yako watu wa mataifa mbalimbali. Hii dunia usipofanya kitu utakufa ujafanya chochote maana kuna watu lazima watakupiga vita hata usipofanya.

Unaweza kusikia jambo umeanza ndio kama unaharibu usiogope anza kufanya hapo hapo hata kama watakucheka maana hao hao kuna siku watakushangilia ukiona vema Roho akakujia fanya uonavyo maana Bwana yuko na wewe. Watu walinicheka sijui kuhubiri naongea ongea tu mbona hawaki, na sikuacha nasiachi maana kuna mahubiri ya anayewaka na asiyewaka. Kuna mambo unatakiwa ufanye na utapigwa vita ila usiache hata wakikutisha. Mungu anamwambia Yeremia nimekuita ila watashindana na wewe ila hawatakushinda.

Mungu akujilie lile eneo ambalo umeitiwa muombe akuongoze kwa Roho wake wa nguvu mwite naye atakuonyesha mambo. Yesu akabatizwa akaanza kuomba kwa nguvu, Roho akamuongoza kwenda nyikani peke yake akarudi katika nguvu za Roho mtakatifu akaanza kuhubiri neno la Mungu. Watu wakamshangaa wakasema huyu si alikuwa seremala imekuwa je? ukijazwa na Roho wa Mungu unakuwa watofauti kabisa utawashangaza wote maskini na matajiri unayaweza mambo yote katika yeye atutiaye nguvu huyu Roho atakusaidia kuona mambo na kutenda kama Mungu anavyoona. AMEN.

 

 

 

Post a Comment

0 Comments