google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

BARAKA YA MUNGU

UFUFUO NA UZIMA UBUNGO CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 30 JULAI 2023 
ASKOFU DKT JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: BARAKA YA MUNGU

Baraka ya Mungu ni nini? Tunaposema mtu kabarikiwa mara nyingi tunaangalia ana magari kiasi gani, nyumba kiasi gani, nguo n.k. Mungu akikupenda hakupi pesa wala mali bali baraka ambayo itakupa pesa na mali. Ayubu alikuwa na mali zote lakini shetani alianza kushughulika vyote alivyokuwa navyo kwa ruhusa ya Mungu. 

“Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao. BWANA akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo. Kisha BWANA akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha BWANA bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi. Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako. BWANA akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa BWANA.” Ayubu 1:6-12.

Ayubu alianza kupoteza mwilini kumbe makubaliano yalishafanyika rohoni kati ya Mungu na shetani. Matukio yote yaliyompata Ayubu yalianzia rohoni kwa mamlaka ya rohoni. Lakini pamoja na kupoteza vyote Ayubu alijua kwamba baraka sio vitu alivyokuwa navyo bali baraka ili leta vitu.  

Ilifika mahali mpaka marafiki zake ambao ni wacha Mungu wakaanza kumhukumu kuwa Ayubu kamuacha Mungu. 

Duniani wapo rafiki wa aina tatu;

  •  Comrade – Urafiki wenu ni kwa sababu mnapigana na adui mmoja. Aina hii ya urafiki utavunjika huyo adui akiondoka. (You share a common enemy)

  • Constituents – Rafiki anayetafuta kile unachotafuta. Mfano ni mfanyabiashara na wewe mfanyabiashara wote mnatafuta hela inapelekea mnakuwa marafiki. (He/She is for what you’re for)

  • Confidant – Rafiki ambaye ukifika kwake unamwambia siri zako zote na asimwambie mtu. Rafiki anayeweza kukukemea, kukupa pole na asimwambie mtu. Huyu ndiye rafiki wa kweli ambaye atakuwa na wewe wakati wa kilio chako na wakati wa kicheko chako

Yesu ni confidant wa watu wote aliowafia msalabani na kuwaokoa. 

“Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi. Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo. Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu. Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni. Haya nawaamuru ninyi, mpate kupendana.” Yohana 15:12-17.

Baada ya yote Mungu alimrudishiwa Ayubu vyote alivyopoteza. Kilichorudisha vyote ni baraka.

“Kisha BWANA akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; BWANA naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza.” Ayubu 42:10.

Kanuni ya neno limetajwa wapi ndio linaonyesha umuhimu yake. Baraka kwenye Biblia inaanza kuonekana kwenye kitabu cha mwanzo.

“Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.” Mwanzo 1:26-28.

Kanuni ya kwanza, kubariki ni kusema. Baraka ni kusemewa/ kuambiwa maneno sawa na upoambiwa maneno kinyume ndio laana. Lile neno linaanza kusababisha matukio kwenye ulimwengu wa roho bila wewe kujua. Magari, nyumba, afya, familia bora n.k sio baraka ila ni matokeo ya baraka. 

Elisha alitamka maneno ya laana, na maneno yale yakazaa dubu wakawala watoto. Baraka na laana yote hutokea baada ya maneno.

“Akakwea kutoka huko mpaka Betheli; naye alipokuwa akienda njiani, wakatoka vijana katika mji, wakamfanyizia mzaha, wakamwambia, Paa wewe mwenye upaa! Paa wewe mwenye upaa! Akatazama nyuma akawaona, akawalaani kwa jina la BWANA. Wakatoka dubu wawili wa kike mwituni, wakawararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao.” 2 Wafalme 2:23-24.

Kanuni ya pili, mdogo hubarikiwa na mkubwa, mdogo hawezi kumbariki mkubwa. 

“Wala haikanushiki kabisa kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa.” Waebrania 7:7.

Maneno unayotamkiwa na mkubwa ndio yanayoamua mwisho wako. Israeli yaani Yakobo aliwabariki Efraimu na Manase hata kama hakuwa baba yao, lakini maneno ya baraka aliyotamka Israeli yaliwabeba pia.

“Israeli akawaona wana wa Yusufu, akasema, Ni nani hawa? Yusufu akamwambia babaye, Hawa ni wanangu, Mungu alionipa hapa. Akasema, Tafadhali uwalete kwangu nami nitawabariki. Na macho ya Israeli yalikuwa mazito kwa uzee, wala hakuweza kuona. Akawaleta kwake, naye akawabusu, na kuwakumbatia.” Mwanzo 48:8-10.

“Akawabariki siku ile akasema, Katika ninyi Waisraeli watabariki, wakisema, Mungu na akufanye kama Efraimu na Manase. Akamweka Efraimu mbele ya Manase” Mwanzo 48:20.

Yakobo aliyaumba maneno ya baraka kwa wanae. (Mwanzo 49:1-28)

"BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA NZIMA YA JUMAPILI"

Post a Comment

0 Comments