google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MATUKIO KATIKA DAMU YA UKOO

UFUFUO NA UZIMA UBUNGO CATHEDRAL 
IBADA YA JUMAPILI 27 AGOSTI 2023 
ASKOFU DKT JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: MATUKIO KATIKA DAMU YA UKOO.

Tumetoka kwenye koo na historia tofauti (we come from different background) kwa namna ya mwili. Yapo matukio yanayotembea kwenye damu ya kila ukoo, ni kama vile unavyoambiwa unafanana na Baba, Mjomba nk. 

Kuna koo na familia zinapitia matukio au matatizo yanayofanana, na matukio hayo ndio matukio katika damu ya ukoo. Kwenye Biblia tunaona ukoo unaongelewa kwenye kitabu cha Mathayo cha ukoo wa Yesu. 

“Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.” Mathayo 1:1.

“Yakobo akamzaa Yusufu mumewe Mariamu aliyemzaa YESU aitwaye Kristo.” Mathayo 1:16.

Kama vile kuna kitabu cha ukoo wa Yesu vivyo hivyo kuna kitabu kinachomuhusu kila mtu kwenye ukoo aliotokea kwenye ulimwengu wa roho. Yesu kwenye mwili anatoka kwenye ukoo fulani ambao una matukio yalioufata huo ukoo yawe mazuri au mabaya.

Ukoo unaotokea una uhusiano mkubwa na hatima yako. Matukio yanayokupata yamesukwa ndani ya damu ya ukoo unaotokea. Kuna matukio yanayofuata kila ukoo yawe mazuri au mabaya, na ili kurekebisha kitabu cha matukio ya damu ya ukoo wako ni lazima utumie damu ya Yesu.

Kuna mambo yanayoufuata mwili uliozaliwa kwenye uko fulani, hivyo basi ni ngumu roho kufikia hatima iliyoandikwa kuhusu wewe. Lile ganda la nje yaani mwili ndio linalokupa shida maana limezaliwa ndani ya ukoo fulani wenye maagano na matukio fulani.

“yaani, habari za Mwanawe, aliyezaliwa katika ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili,” Warumi 1:3.

"BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA NZIMA YA JUMAPILI"

Somo la leo linapatikana kwenye Kitabu cha "MATUKIO KATIKA DAMU YA UKOO". Wasiliana nasi kupata nakala yako kupitia maelekezo yafuatayo.




Post a Comment

0 Comments