google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KUKOMESHA MATUKIO YA SHETANI

 

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 30.11.2025
ASKOFU DKT GESHOM MWAKILA
SOMO: KUKOMESHA MATUKIO YA KISHETANI

Dunia imejaa matukio tofauti, na ndani ya matukio hayo yamegawanyika katika makundi mbambali. Kuna matukio ya furaha, matukio ya kupata, na matukio ya kukosa pamoja na matukio mengine mbalimbali.

Kwa kila jambo kuna majira yake,Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa; Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza;Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga; Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza; Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe;Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza;Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa; Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;”   Mhubiri 3:1-7

Nyakati zimebeba matukio mbalimbali, kama vile wakati wa kupata ambao huambatana na matukio ya kupata. Wakati wa mtu wa kupata unapofika, ni lazima matukio fulani ya kupata yatokee ndani ya maisha ya mtu huyo. Kwenye maisha ya kila siku asili ya mtu huwa ni katika ulimwengu wa roho. Hivyo hata wakati huwa unaanzia kujulikana rohoni ndipo matukio fulani hutokea kwenye ulimwengu wa mwili.

“Nyakati zako zitakuwa nyakati za kukaa imara; za wokovu tele na hekima na maarifa; kumcha BWANA ni hazina yake ya akiba.” Isaya 33:6

Kwa asili mtu ni roho ambaye yupo ndani ya nyumba ambayo inaitwa mwili. Watu wakitaka kutengeneza matukio huwa wanashughulika na ulimwengu wa roho, na baada ya hapo matukio yanaonekana kwenye ulimwengu wa mwili. Wachawi ili waweze kutengeneza matukio juu ya mtu wanashugulika kwenye ulimwengu waroho ambao ni ufalme wa giza.

Ulimwengu wa roho umegawanyika katika makundi mawili au falme mbili, kuna ulimwengu wa roho wa nuru na ulimwengu wa roho wa giza. Ulimwengu wa nuru una nguvu kuliko ulimwengu wa giza. Mtu ambaye yupo kwenye ulimengu wa roho wa nuru una uwezo wa kuharibu ufalme wa giza. Kila matukio yanayo tengenezwa katika ufalme wa giza yanaweza kuharibiwa na ulimwengu wa nuru. Ulimwengu wa nuru uaongozwa Mungu aliyembinguni na ulimwengu wa roho wa giza unaongozwa na shetani.

Kuna matukio ambayo yanaonekana kuwa ni ya kawaida ila yanakuwa yametengenezwa na mtu. Kunakuwa na mtu ametamka maneno kwenye ulimwengu wa roho, na nyuma ya neno hilo huwa kuna roho. Roho inasubiri neno ili kulipa uhai neno hilo. Kunakuwa na viumbe vimesetiwa kusikiliza hilo neno ili kulitimiza katika upande wa Mungu ama wa Shetani. Mtu akipakwa mafuta haijalishi muonekano wake, Mungu humtofautisha mtu huyo na watu wengine.

Sio kila matukio yanayotoka mbinguni huwa ni ya Mungu, kuna mengine yanatoka kwa Shetani. Katika biblia inaonesha Shetani aliteketeza mali za Ayubu kwa moto kutoka mbinguni, hii inaonesha kuna matukio ambayo yanatoka mbinguni ila Shetani ndio aliyesababisha.

Kwenye ulimwengu wa kiroho kuna mawakala wa aina mbili ambao ni mawakala wa mambo mema na mawakala wa uharibifu. Mawakala wa mambo mema wanatoka kwa Mungu na mawakala wa uharibifu huongozwa na Shetani. hivyo unatakiwa kuwafahamu mawakala wa uharibifu kwa kufanya vita katika ulimwengu wa roho nao ni kwa kuomba.

"Kisha nikaona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka katika nchi; naye alikuwa na pembe mbili mfano wa Mwana-Kondoo, akanena kama joka. Naye atumia uwezo wote wa mnyama yule wa kwanza mbele yake. Naye aifanya dunia na wote wakaao ndani yake wamsujudie mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.” Ufunuo13:11-12                                                                                                                                                                                                                                                                                               

Post a Comment

0 Comments