google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

NGUVU YA MSALABA SEHEMU YA PILI

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 21.12.2025
ASKOFU DKT GESHOM MWAKILA
SOMO: NGUVU YA MSALABA SEHEMU YA PILI

Sehemu ya kwanza tulijifunza kwamba msalaba ni nguvu ya wokovu na kaburi lililo wazi inamaanisha kuwa kanisa limeshinda mauti. Nguvu ya msalaba inabeba vitu vifuatavyo: Inabeba msamaha, Inakupa uhakika kwenye mambo ya maisha yako, Inatupa kukubalika.

Kwa kila kazi ambayo mtu anafanya, upo mshahara wa kazi hiyo. Ukifanya kazi ya Mungu sawasawa na alivyokupa, kuna mshahara wake ambao anakupatia. Vivyo hivyo  ukifanya kazi ya Mungu kwa uzembe na ukiwa unajua kuwa hufanyi sawasawa na mapenzi ya Mungu, pia utalipwa mshahara sawa sawa na kazi yako.

 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.” Ufunuo 22:12

Kila mtu anaefanya kazi kwa mwajiri fulani, basi mwajiri wake ndio mwenye dhamana ya kumlipa mtu huyo mshahara. Ukifanya kazi ya Shetani atakaye kulipa ni Shetani, na ukifanya kazi ya Mungu utalipwa na Mungu. Neno la Mungu linaweka wazi kuwa, msahara wa dhambi ni mauti. Ila kwa kupitia kupigwa kwa Yesu msalabani, alichukua dhambi ya ulimwengu. Yesu alichukua dhambi zako ili wewe uweze kukubalika kwa Mungu. Kwa nguvu ya msalaba wa Yesu inakupa kukubalika na kupatana tena na Mungu.

5.MSALABA WA YESU UNAKUPA UPATANISHO 

Kwa nguvu ya msalaba wa Yesu, inakupa kupatana na Mungu pamoja na watu wengine. Kwa nguvu ya upatanisho iliyo katika msalaba wa Yesu, inakufanya mpatane tena na kuwa na umoja na mtu ambaye mlikuwa hampatani. Msalaba wa Yesu ni nguvu ya upatanisho baina ya watu. Msalaba wa yesu unaleta neema ya upatanisho baina ya watu.

“Na penye msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mamaye, na umbu la mamaye, Mariamu wa Klopa, na Mariamu Magdalene. Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao. Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake.” Yohana 19:25-27

Mungu ni mmoja na mpatanishi ni mmoja ambaye ni Yesu Kristo. Yeye ambaye ametoa uhai wake ili kuupatanisha ulimwengu wote na Mungu, na upatanisho wa mtu na mtu. Yesu ni mpatanishi kati ya mtu na Mungu. 

“'Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu;” 1Timotheo 2:5

6. MSALABA WA YESU UNAKOMESHA MATESO

Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, Imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake.” Yohana 19:30

Yesu alidhalilishwa na kuaibika mbele ya watu. Ila hayo aliyaruhusu ili watu walio mpokea wasiaibishwe tena bali wapte heshima. Yesu ndie mtu ambaye ameaibishwa kwa asilimia zote, lakini ndiye ambaye Mungu akamwinua juu sana kuliko vitu vyote. Ila kuinulia kulikuja baada ya kunyenyekea na kustahimili aibu. 

“ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.” Wafilipi 2:10-11

Unyenyekevu unaleta kuinuliwa. Unyenyekevu unaleta kibali kwa Mungu, naye Mungu atakuinua na jina lako litakuzwa. Yesu alikuwa mnyenyekevu wa kufanya mapenzi ya Mungu na Mungu akampa jina lipitalo majina yote.

“jambo lile ninyi mmelijua, lililoenea katika Uyahudi wote likianzia Galilaya, baada ya ubatizo aliouhubiri Yohana; habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.” Matendo 10:28

Kupitia msalaba wa Yesu Kristo kuna nguvu ya kufufua wafu kutoka kwenye makaburi, na pazia la hekalu likapasuka.

7.MSALABA WA YESU UNAFUTA HATI ZA MASHITAKA 

Kila mtu alieokoka ni raia wa Mbinguni. Maisha ya kiroho yana mshtaki ambaye ni kiumbe wa rohoni katika ufalme wa giza. Kazi yake ni kumshtaki raia wa mbinguni pale anapofanya kosa. Kuna sheria ya mbinguni inayomruhusu mshtakiwa amshitaki raia wa mbinguni na anapeleka mbele za Bwana. 

“Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;” Wakolosai 2:13

Lakini kupitia nguvu ya msalaba wa Yesu, mashitaka yote yalifutwa. Kupitia msalaba wa Yesu, hati ya mashitaka iliondolewa na hukumu nayo ikaondoka. Pasipo mashitaka hakuna hukumu. Yesu alipokuwa anasulubiwa, alifuta mashitaka ya ulimwengu ili watu watakao mpokea yeye wasishtakiwe.

Mshtaka hayo yanaondolewa kwa watu ambao wamemkiri Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao. Mtu anapo mkiri Yesu, anapokea nguvu kutoka kwenye msalaba ambayo inaondoa hukumu na adhabu ya mashitaka. Pale usipo mwamini Yesu, unakuwa na vazi ambalo linamaana ya kuhukumiwa. Kuna mambo yanampata mtu na yanamtesa ni kwasababu ya kutomwamini Yesu, na kutopata ile nguvu ya msalaba yenye kufuta mashitaka.

“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.”

Yohana 3:16-19


Post a Comment

0 Comments