google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KULITUMIKIA KUSUDI LA BWANA KWENYE KIZAZI CHAKO

UFUFUO NA UZIMA CATHEDRAL
IBADA YA JUMAPILI 27.12.2025
ASKOFU BARAKA THOMAS TEGGE
SOMO: KULITUMIKIA KUSUDI LA BWANA KWENYE KIZAZI CHAKO

Mungu ni roho na mtu ni roho. Kila mtu aliye juu ya uso wa nchi ameletwa na Mungu. Alimleta kwa kazi maalumu ili kutimiza kusudi lake. Kufanikiwa kufanya kusudi la Mungu sio kuwa na nyumba nzuri, au pesa au watoto, ila kufanikiwa ni kulifanya kusudi alilokutuma. Kuna watu mawazo yao ni mawazo ya Mungu, na nia yao ni nia ya Mungu.

“Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi ilivyo kubwa jumla yake!” Zaburi 139:17

Watu wengi hudhani kumiliki vitu ni muhimu sana. Mtu anaweza kufanya jambo la kumkosea Mungu, ili tu aweze kumiliki vitu fulani. Lakini hii ni kwa sababu watu hawatambui kuwa, mtu ni roho hivyo kila kitu alichonacho kwenye ulimwengu huu atakiacha. Zile mali, pesa, magari, muonekano na mwili ulionao vyote utaviacha, nawe utarudi ulipotoka. Nawe utaenda kupeleka ripoti kwa mambo unayoyafanya mbele za  Mungu kutokana na kusudi alilokutuma kufanya.

“Na alipokwisha kumwondoa huyo, akamwinua Daudi awe mfalme wao ambaye alimshuhudia, akisema, Nimemwona Daudi, mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayefanya mapenzi yangu yote.” Matendo 13:22

Andko hili linaonesha Mungu humweka na kumtoa mtu yoyote kwa ajili ya kusudi lake. Kila kitu ambacho Mungu anakupatia ni ili kitumike kutimiza kusudi lake. Mtu mwenye akili anajua kuwa anaishi hapa kwa muda tu. Hivyo anatambua kuwa muda wake ni mchache, anafanya mambo yake yote ili kulitimiza kusudi lake ndani ya muda.

Wakati ukifika wa kuondoka duniani, utaondoka hata kama bado hujamaliza kusudi la Mungu. Ndomaana Mungu hutukumbusha kuukomboa wakati. Maisha ni mfano wa mtu ambae yupo kwenye chumba cha mtihani, muda wakumaliza mtihani ukifika ukiwa umemaliza au haujamaliza lazima utakusanya na kusubiri matokeo.

“Kwa kila jambo kuna majira yake,Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa;Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;”Mhubiri 3:1-4

Mungu humchagua yoyote amtakaye hata kama hafai machoni pa mtu. Kuna nyakati mambo kama vile chuki ama kusalitiwa, ni mpango wa Mungu ambao ni sehemu ya kutengeneza kwaajili ya kufanya kusudi lake.

“Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.” Warumi 8:18

Ukitaka kuamua mambo usitake ushauri wa watu, ukishawishika kufanya jambo fulani, lifanye bila kusikiliza ushauri kutoka kwa watu. Maana kuna ushauri wa watu unakuzuia usilifanye lile kusudi la Mungu.

“Kwa kuwa mimi sikushuka kutoka mbinguni ili niyafanye mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenipeleka.” Yohana 6:38

Kuna mambo unatakiwa ufanye jambo kwa bidii kwa maana ni muda tu, usipoteze kusudi kwa ajili ya mtu, inakubidi ulifanye kusudi la Mungu kwa bidii ili uweze kuikamilisha mapenzi ya Mungu.

1.    Kusudi la Mungu ndio sababu mama la wewe kuwepo duniani. Ukiwa duniani yapo mambo mengi yakuafanya, ingawa kuna vitu ukikosa haina shida ila ukishindwa kulifanya kusudi la Mungu ni umepoteza kila kitu. Kusudi lilitangulia kabla ya wewe kuwepo duniani.

“Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.” Yeremia 1:5

2.    Kusudi la Mungu halizuiliki, Mungu hutangaza mwisho wa mtu hata kabla ya mwanzo wake. Mungu akiwa na jambo, hakuna awezaye kulizuia. Kuna mambo unahisi kwamba ni kikwazo cha kuzuia usifanye kusudi la Mungu, ila ni Mungu anaruhusu ili liweze kukupeleka kwenye kusudi la Mungu.

“Wakamwona toka mbali, na kabla hajawakaribia, wakafanya shauri juu yake ili wamwue. Wakasemezana wao kwa wao, Tazama, yule bwana wa ndoto anakuja. Haya, twende, tukamwue na kumtupa katika birika mojawapo, nasi tutasema, Mnyama mkali amemla; kisha tutaona zitakuwaje ndoto zake.” Mwanzo 37:18-20

 Kupingana na mtu mwenye kusudi la Mungu, ni kupigana na Mungu. Na kila anayepigana na Mungu, hupondwa kabisa. Moja ya sababu ya kifo kabla ya wakati, ni kupingana na kusudi la Mungu juu ya mtu.8\

“Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa, 39lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu.” Matendo ya mitume 5:38-39

BONYEZA HAPA KUANGALIA IBADA YA JUMAPILI

Post a Comment

0 Comments