google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Matukio ya Jumapili, 18 Aprili 2010 Katika Picha


Kijana Barnaba aliyekuwa msukuleni na baadaye kuokolewa na BWANA Yesu, akimsifu BWANA Yesu kupitia kibao cha wimbo wake unaokwenda kwa jina la “niliteswa”. Pamoja naye katika picha wakimtukuza BWANA Yesu ni Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima. Nyuma katika picha ni watu wanaume,wanawake na watoto waliokuwa msukuleni nao pia wakiungana na Kijana Barnaba Kumsifu na Kumtukuza BWANAYesu katika anga la uweza wake.


Makutano makubwa wakimwabudu YEHOVA katika ibada ya jumapili ya leo 18 Aprili 2010, katika viwanja vya Tanganyika packers ambapo ndipo lilipo kanisa la Ufufuo na Uzima, kawe jijini Dar es Salaam.

: Binti, aliyefufuka kutoka kwa wafu akishuhudia uweza na nguvu za BWANA Yesu. Binti huyu mara baada ya kufa tu kaka yake alianza kuomba maombi ya kumrudisha akilitaja jina la Yesu akisema rudisha katika Jina la Yesu na kupambana katika maombi ya nguvu kwa muda wa masaa sita(6) na hatimaye dada yake alifufuka.



Kaka wa binti aliyekufa na baada ya maombi kufufuka, akieleza namna alivyokuwa akiomba maombi ya kumrudisha dada yake mara tu alipokufa.


Kijana kutoka Tanzania, nyumba ya Ufufuo na Uzima, Daniel akiwa katika picha ya pamoja na mkewe Bi Akali kutoka japani. Pamoja nao katika picha ni Wazazi wa Akali waliotoka Japani kuja kushuhudia mtoto wao akifunga ndoa katika nyumba ya Ufufuo na Uzima. Katika picha pia ni Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima wakiwa na wachungaji wengine kwa pomoja wakimtukuza BWANA Yesu mara baada ya ndoa hiyo kufungwa hapa kanisani.
Shetani akiaibishwa......

Familia ya Happiness Kahabi katika picha. Wa kwanza ni mama yake mzazi, anayefuata ni kaka yake ambaye ni Daktari wa meno, Happiness mwenyewe wapili kutoka kulia na wa kwanza kulia ni mume wake.


Kijana Emmanuel aliyekufa kwa kujinyonga huko Moshi mkoani Kilimanjaro na hatimaye kufufuka akishuhudia jinsi hali ya mambo ilivyokuwa mara baada ya kujinyonga, kufa na baadaye kufufuka.
Mbongo Akijitwalia jiko la Kijapani.....
Kijana Daniel akimvisha pete ya ndoa mkewe Bi Akali ndani ya Nyumba ya ufufuo na Uzima.

Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima akiwa na wachungaji wengine wakiwaombea Daniel na Akali mara baaya ya ndoa yao kufungwa katika nyumba ya Ufufuo na Uzima, ndani ya viwanja vya Tanganyika packers vilivyopo kawe, Jijini Dar es Salaam.

Post a Comment

0 Comments