google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Ujumbe : VYANZO VIWILI VYA NGUVU YA MUNGU.

Na. Mch. Kiongozi Josephat Gwajima. 25 Machi, 2012

NGUVU ni uweza au mamlaka ya kufanya jambo Fulani, sisi kama wakristo tunahitaji nguvu ya kutuwezesha kutenda mapenzi na kazi za Mungu duniani, na Biblia inasema hatuwezi kutenda , kwa usahihi duniani kama hatuta kuwa na nguvu za Mungu, 2 Wakorintho 2 :4…., Wakorintho 4:20, unapoongelea ukristo unaongelea nguvu kwa maana ukristo ni nguvu. Injili ya Yesu kristo imejengwa katika nguvu za MUNGU. Tofauti kati ya ukristo na dini nyingine ni nguvu iliyo ndani ya jina la Yesu..

Kama tulivyoona ukristo sio maneno matupu tu au tunavyokili bali ukristo umejengwa kwenye nguvu ya Mungu.. nguvu kuponya, kufufua, kufungua na kuokoa.. na ndio maana mtume Paulo anasema kwenye kitabu cha Wathethalonike 1:8.. kuhubiri kwetu hakukuwa katika maneno bali katika Nguvu ya Mungu.. 1 Timotheo 1:7 ´´Mungu hakutupa roho ya hofu bali roho ya nguvu´´ na ndio maana biblia inasema kuwa ´´nanyi mtapokea nguvu akishawajilia juu yenu roho mtakatifu´´

Yesu yu hai, na ana nguvu, Yesu wetu hayupo kaburini, alifufuka ..hayupo ndani ya tumbo la bikira Maria bali yupo hai mbinguni na anatenda kazi duniani.. Waefeso 3:20.. ´´ kulingana na NGUVU itendayo kazi ndani yetu´´ ndani ya kila mtu aliyeokoka kuna nguvu ya Mungu.. Waefeso 6:10 ´´katika uweza..¨ uweza unamaanisha nguvu.. YESU ALITUPA NGUVU HIZO ambazo twazipata kupitia vyanzo viwili..

NGUVU YA MSALABA WA YESU KRISTO..

Unaweza kujiuliza kwanini ukiweka msalaba wa Yesu kwenye nchi kama Iran, au nchi nyingi za kiarabu utapingwa sana na unaweza hata kuuawa, Hii ni kwasababu msalaba wa Yesu kristo una nguvu.. kuna nguvu ipatikanayo kwenye msalaba inaitwa ¨NGUVU YA MSALABA¨ 1 Wakorintho 1:18 ¨ujumbe wa msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi lakini kwetu sisi tunaoamini ni nguvu ya Mungu¨ kumbe kwenye msalaba wa Yesu Kristo kuna uweza uletao wokovu. Msalaba wa Kristo una nguvu.

Kwanini ujumbe wa msalaba unabeba nguvu?,

Unaweza kujiuliza ni kwanini, iwe nguvu ya msalaba na isiwe nguvu ya kitu kingine kama jua, mwezi, dunia au nabii.. mfano : nilisoma (Mch. Gwajima) kitabu kimoja kuhusu ajali ya ndege, ambayo rubani aliwatangazia watu kuwa ndege inaanguka na kila mtu alishauriwa kuandika mambo aua ujumbe kwa ajili ya familia au watu anao waacha duniani.. ukijaribu kuwaza wakati huu utagundua mtu awezi kuandika non-sense pale , maana ni wakati wa mwisho. Kila mtu ataandika jambo la muhimu ambalo angehitaji watuanaowaacha wajue.

Kwa mfano huo, tunaweza kuona kuwa maneno saba ya mwisho ya Yesu Kristo kabla ya kufa ni maneno ya muhimu na nguvu ya msalaba imejengwa kwenye maneno yale.. ni muhimu kujua Yesu alipigwa kwa ajili Yetu.. na magonjwa na matatizo yetu yalipigwa pamoja naye.


MANENO 7 ALIYOYASEMA YESU KABLA YA KUFA..


i.) Mathayo 27:46, Kwa wakati ule alibeba dhambi zetu zote. Na ndio maana Mungu akamwacha pale msalabani tunajua kuwa Mungu alimwacha kwa maneno ambayo Yesu alitamka akisema ´´ baba mbona umeniacha´´ baada ya Yesu kubeba dhambi za ulimwengu, Mungu akamwacha na Yesu akasurubishwa kwa dhambi ambazo hakutenda bali alitenda.. Yesu alisulubiwa kwa makosa YETU..


ii.) Luka 23: 34 -Katikati ya maumivu Yesu alisamehe.. watu wa dunia wanaweza kukwambia nimekusamehe lakini sitasahau lakini Yesu akiwa msalabani na katikati ya maumivu makuu ya msalaba akasema ´´baba wasamehe maana hawajui walitendalo´´ ZABURI 103:3 Nguvu ya msalaba unatupa nguvu ya kusamehe, kuna watu wengi wapo kwenye matatizo kwasababu ya kuto kusamehe.. ni kanuni ya Mungu kusamehe na kuponya . tunajifunza hili kwa wale waliomleta mtu kwa Yesu , mgonjwa akiwa kwenye godolo.. na Yesu kabla ya kumponya alimtangazia msamaha wa dhambi kwanza na baada ya hapo akamponya.. Kumbe msalaba unatuwezesha kusamehewa..


iii.) Luka 23:42-43 - ¨..Leo utakuwa pamoja nami peponi ..¨ hili ni neno ambalo Yesu alimwambia mmoja kati ya wale wanyang´anyi, akimwambia kuwa tutakuwa wote peponi, Yesu alisurubiwa pamoja na wanang´anyi.. kumbe usitishe na mtu anaye vaa msalaba akasema ni mtu wa Mungu, kwasababu wengine wanaweza kuvaa msalaba wa wanyang´anyi.. na kwa andiko hili tunajifunza kuwa nguvu ya msalaba inatupa nguvu ya kukumbukwa kwenye Ufalme wa Yesu.. kumbe msalaba unatupa nguvu ya kukumbukwa .. Mungu anakumbuka maombi yako, kazi yako, maisha yako na hata taifa lako.. Mtu yeyote awezi kukuhakikishia kwenda na kuuona ufalme wa Yesu isipokuwa msalaba wa Yesu ndio unaotupa uwakika wa kuuona Ufalme wa Mungu ´´hakuna jina jingine duniani, litupasalo kuokolewa kwalo isipokuwa jina la Yesu..


iv.)Luka 23:46, Kwa mtu yeyote aliyeokoka ,amekabidhiwa kwenye mikono ya Yesu kristo.. na hutakufa mpaka siku ya Bwana , kwasababu roho yako imekabidhiwa kwenye mikono ya Yesu Kristo.. huu ni ulinzi ambao kila mtu aliyeokoka anakuwa nao.. tupo mikononi mwa Mungu na hakuna mtu awezaye kututoa kutoka katika mikono ya Yesu Kristo..


v.) Yohana 19:29 Yesu akiwa msalabani , alikuwa anajali mahusiano.. hii inaonyesha kuwa msalaba wa Yesu unatupa usalama ndani ya mahusiano na wazazi na watu wengine.. Msalaba wa Yesu unatupa mahusihano bora . ukimwomba Mungu akupe nguvu ya mahusiano.. Kumbe msalaba ulileta Nguvu ya upatanisho.. Nguvu ya msalaba inaleta watu pamoja , watumishi wa Mungu pamoja, familia pamoja.. ujumbe wa msalaba ni upuuzi kwao wasioamini lakini kwetu sisi ni NGUVU YA UPATANISHO.


vi.) Yohana 19:28 ¨..ninasikia kiu..¨ hapa Yesu alikuwa amekaa msalabani kwa muda , na alisikia kiu.. kwa kuwa hakuwa amekunywa maji.. kumbe msalaba wa Yesu unakupa kiu ya kumtafuta Mungu, kiu ya kuomba, kiu ya kuponya na kuokoa na rahisi kusikia watu wakisema nyinyi watu wa ufufuo na uzima kwanini kila kitu mnataka mtende nyinyi.. ni muhimu kujua kuwa msalaba wa kristo unatupa kiu ya kutenda na kuthibitisha nguvu ya Mungu.. na inawezeka ulipokuwa umeokoka ulipata hamu sana ya kuomba na kumtafuta Mungu..lakini baada ya muda ile kiu imepotea basi kama unatatizo hilo ni wakati wa kwenda mbele ya msalaba wa Yesu kristo.. na kuomba KIU ya kumtafuta Mungu na Mungu atakupa.. unaweza kuniuliza mimi( Mch. Gwajima) kiu yako ni nini? Mi nitakwambia kiu yangu ni kuona watu milioni moja wanakuja ndani ya ufufuo na uzima Dar es salaam.. nah ii ni kiu nilionayo… kuwa dunia iokolewe na waarabu waokolewe.. ninaona njia kuu ya udhihirisho wa nguvu ya Mungu itakayo tikisa mataifa kutoka katika msalaba wa Yesu.. Nguvu ya msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi lakini kwetu sisi ni KIU YA KUMTAFUTA MUNGU.

vii.) Yohana 19:30 ´´.. Yesu alipopokea kile kinywaji akasema IMEKWISHA´´ Kimsingi hakuna aliyemuua Yesu bali aliutoa uhai wake , ili aupokee tena.. na kimsingi Yesu alitenda mambo makubwa ya ufalme wa Mungu, na kwasababu hiyo shetani akakusanya watawala na watu wamuue Yesu na alipokuwa msalabani na kupiga kelele kusema imekwisha.. shetani akafikiri kuwa amemuangamiza na inawezekana kabisa kule kuzimu mashetani walianza kushangilia na inawezekana hata wachawi wa kipindi kile walienda kwenye sherehe .. lakini katikati ya sherehe yao. na Yesu akiwa nanig´inia msalabani Yesu akasema IMEKWISHA..

Baada ya Yesu kusema kuwa IMEKWISHA.. BIBLIA inasema

I. Dunia ikatikisika,.. kumbe Nguvu ya msalaba inaweza kutikisa dunia,
II. Makaburi yakafunguka, miili mingi ya watakatifu wengi ikafufuka. Kumbe Nguvu ya msalaba yaweza kurudisha. Na ndio maana mimi nashangaa watu wanaokataa kuwa wafu hawafufuki..najiuliza ni msalaba gani wanao uhubiri.. labda ni misalaba ya wale wanyang´anyi ..
III. Miamba ikavunjika kumbe msalaba wa Yesu unaweza kuvunja miamba.
IV. Jua likatiwa giza
V. Pazia la hekalu likapasuka.


KWELI KADHAA KUHUSU NGUVU YA MSALABA..


Kipindi cha zamani kulikuwa na aina za usulubishaji.. aina ya kwanza ni ya mti mmoja kama namba moja, ya pili ilikuwa alama ya kuzidisha yaani ´X´ , tatu ni wa alama ya T, na alama ya kujumlisha nah ii inamaanisha msalaba wa Yesu unatupa kujumlisha , kuongezeka, na kukua.. sisi tumesulubishwa pamoja na kristo

Yesu alisurubishwa kwenye mlima, na mahali pale kila mtu aliweza kumuona ,, watu kutoka kila mahali walimuona.. kumbe Yesu alisurubiwa mlimani ili kila mtu aone nakama Yesu alivyoinuliwa mlimani ili kila mtu amuone..´´kama vile Musa alivyomuinua nyoka jangwani mwana wa adamu naye aliinuliwa..

Na unagundua watu walimuona Yesu akisurubiwa mbele ya watu, njiani, mlimani na alipo taka kupaa akaenda mlimani pia..ili watu wote wamuone,, kumbe kama ulikuwa chini na watu walikuona chini Msalaba wa Yesu utakuinua mbele ya watu wote walikuona ukiahibika..

Yesu akashuka kuzimu katika zile siku tatu alipokuwa amekufa, akamnyang´anya funguo za mamlaka.. na hapo akamkanyaga kichwa shetani .. kutimiza andiko ´´uzao wa mwanamke utamkanyaga nyoka kichwa´´



NGUVU YA KABURI LA KRISTO LILILO WAZI..

Hii ni nguvu tunayoipata kutoka katika nguvu ya kaburi la kristo.. kwa maana malaika alikuja kaburini na kukuta .. walinzi pale na baada kutetemesha lile eneo .. wakalisukuma jiwe la kaburi na kulikalia na hapo Yesu akafufuka na kutoka kaburini.. nah ii ni nguvu ya ufufuo na baada ya siku chache kabla ya kupaa akatangaza ´´mamlaka yote nimewapa ninyi ..´´ tuna mamlaka ya kuitawala dunia.. Nguvu ya kaburi lililowazi imetupa mamlaka.. sisi tuko ndani ya Yesu na Yesu yupo ndani yetu.. ´´tunalindwa na NGUVU za Mungu kwa njia ya imani..

Baba Josephat Gwajima atakuwepo katikati ya wiki kwa ufafanuzi zaidi wa somo hili.. Mungu akubariki sana..

Post a Comment

0 Comments