Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Rev.Josephat Gwajima ameutangaza mwaka 2013 kuwa mwaka wa kupita katikati ya adui zetu. Akitangaza hayo katika Mkesha wa Mwaka mpya kanisani hapo Mchungaji alisema kuwa "Mwaka huu ni mwaka wa Kupita Katikati Yao"
Ufunuo huu wa kupita katikati yao unatoka katika kitabu cha Luka 4:30 imeandikwa "Lakini Yeye (Yesu) alipita katikati yao, akaenda zake." Yesu alipita katikati ya adui zake nao hawakuweza kumdhuru. Mchungaji alisisitiza kuwa kwa kawaida ukilikwepa jaribu utalikuta mbele, unatakiwa kupita katikati yake. Majaribu yapo namna hiyo. Pita katikati, neema imeachiliwa tayari.
Mishumaa ikiwashwa kwa moto kutokea madhabahuni |
Mchungaji Kiongozi aliyasema hayo katika ibada ya Mkesha ambapo maelfu ya watu walikuwapo kanisani hapo wakimshukuru Mungu kwa neema ya kuingia mwaka 2013 salama. Katika ibada hiyo, ilipotimia saa 6 kamili usiku, taa zote zilizimwa na mishumaa mingi iliyonyanyuliwa juu na kila mtu aliyekuwepo ibadani hapo iliwashwa kwa moto wa mshumaa ulioanzia madhabahuni ikiwa ni ishara kuwa moto wa madhabahuni utawaka mwaka wote 2013 kwa kila mmoja na hautazimika.
Wachungaji wakazi (Resident Pastors) wakiomba kwa ajili ya maombi 10 ambayo kila mshirika aliandika ya kwake ili Mungu amtendee kwa mwaka 2013 |
0 Comments