Na Mwandishi wetu,
Asubuhi majira ya saa tatu asubuhi majeshi ya Bwana
walikutana katika viwanja vya relini,hii ni pamoja na wale waliokua waliofikia
sehemu mbali mbali tofauti na kambini.
Baada ya kufika uwanjani watu wote waligawanywa katika
makundi kumi yaliyokua chini ya ma MP’s , na makundi yote hayo kumi yalikua
chini ya AP.
Baada ya kugawanywa katika makundi imbali mbali majeshi ya
Bwana yalipanda mabasi ya ufufuo na uzima kuelekea mahali ambapo
walitakiwakwenda kubandika matangazo kwa siku hiyo.
Wakati wakielekea huko walipofika njiani eneo la Mrefu
walisimama kwa muda kulisubiri gari la matangazo ambalo lilifika panapo majira
ya saa nane mchana.
Wakati gari la matangazo likisubiriwa maeneo ya Mrefu baadhi
ya watenda kazi walitumia nafasi hiyo kukaribisha watu wa maeneo hayo katika
mkutano unaoanza tarehe 27 /9 /2013.
Baadhi ya mambo yaliyojitokeza wakati huo ni pale baadhi ya
watu walionyesha kiu ya kutaka kumpokea Yesu ,ndipo baadhi ya mashepherd wa
Ufufuo na uzima walipotumia fulsa hiyo kuongoza watu hao sala ya toba na
kuwaombea baadhi yao .
Kati ya mambo yaliyotendeka mahali hapo ni tukio la mamammoja
aliyekua miongoni mwa waliompokea Yesu kushuhudia na kusema alikua akisumbuliwa
na maumivu ya tumbo muda mrefu na alipokwenda hospitali walisema ana vidonda
vya tumbo, lakini baaada ya kuombewa maumivu yaliisha pale pale,
Haikuishia hapo mama mmoja nae aliyekua akisumbuliwa muda mrefu
na matatizo ya miguu alipokea ponyaji wake pale pale na kushuhudia kua maumivu
yaliyokua yakimsumbua yametoweka mara moja.
Tuliondoka mahali pale majira ya saa nane na nusu mchana na
kuwaacha watu wa eneo la mrefu wenye furaha huku wakiahidi kutokukosa katika
mkutano baada yakuona Mungu akiwagusa hao wachache waliokua hapo.
Baada ya hapo tuliondoka na kwenda moja kwa moja katika eneo
la Tengeru, Eneo hili lilikua na watu wengi kidogo kulingana na shughuli mbali
mbali zilizokua zikiendelea mahali hapo.
Majeshi ya ufufuo na uzima yalipofika mahali hapo watu walionekana
kuguswa na matangazo hayo na ndipo waliposogea kwenye gari la matangazo kwa
wingi ili kusikiliza kilichokua kikiendelea hapo.
Tulipoongea na baadhi ya watu kuwakaribisha kwenye mkutano
walionekana kuwa na shauku kubwa yakuhudhuria, huku wengine wakiuliza kanisa
lenu liko sehemu gain hapa Arusha ili tuje?
Maeneo ya Tengeru lilibandikwa tangazo kubwa la mkutano
lenye picha ya baba (SNP JOSEPHAT GWAJIMA)
Na panapo majira saa 11:45 jioni majeshi ya Bwana yalianza
kurudi uwanjani. Wakati tuko njiani kurudi tulifika eneo moja ambapo jina lake halikuweza
kupatikana kwa haraka hapo napo liliwekwa tangazo jingine kubwa barabarani.
Majeshi ya Bwana yakarudi uwanjani panapo majira ya saa moja
usiku wakafika wote uwanjani,.
Mnamo saa mbili usiku majeshi ya Bwana yaliongozwa na Rp
Bryson kufanya maombi na kuzunguka uwanja huku wakipiga majeshi .
Baada ya maombi majeshi ya Bwana walielekea kambini kwaajili
ya kupata chakula cha usiku pamoja na kupumzika
IKAWA JIONI IKAWA ASUBUHI, SIKU YA JUMAPILI
Imetayarishwa na Shepherd Frank John Minja.
Na kuhaririwa na Mp Davie M Abson
0 Comments