google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

IBADA KUTOKA NYUMBA YA UFUFUO NA UZIMA MOSHI



IBADA KUTOKA NYUMBA YA UFUFUO NAUZIMA  MOSHI.                                            
SOMO: DALILI ZA MTU ALIYECHUKULIWA MSUKULE
TAREHE:  29/10/2013.
MCHUNGAJI KIONGOZI: JOSEPHAT GWAJIMA
MCHUNGAJI MWANDAMIZI:MWANGASA

Shetani yupo na anafanya kazi lakini watu wengine hawaamini kama shetani yupo.Mtu anaweza kuingiwa au kutupiwa mashetani asiweze kula wala kunywa.Pia mashetani yanaweza kumfanya mtu akonde na kuwa mwembamba.
Mark 9:18 na kila ampagaapo, humbwaga chini, naye hutoka povu na kusaga meno na kukonda; nikasema na wanafunzi wako wamtoe pepo, wasiweze”.
Pepo anaweza kumwekea mtu kifafa,kutaliwa na laana.Mark 9:20 “Wakamleta kwake; hata alipomwona, mara yule pepo alimtia kifafa; naye akaanguka chini, akagaa-gaa, akitokwa na povu”.

Dalili za mtu aliyechukuliwa msukule.

1.Anaanza kuwatokea jamaa zake baada ya kufariki.Kuwa anaonekana mtu aliyekufa ni dalili ya watu wa familia kuwa na mashetani.

2.Baada ya kufariki anatokea mtu ndani ya familia anang’ang’ania  au kulazimisha mazishi yafanyike siku hiyo hiyo.

3.Baada ya mazishi,siku ya pili au ya tatu kaburi la marehemu huyo linaanza kutitia,hii ni kwa sababu mtu aliyechukuliwa msukule anakuwa bado ndani ya mwili.  

4. Marehemu anaonekana ama mrefu au mfupi sana zaidi ya kipimo cha mwanzo kipindi cha uhai wake.Hapa yawezekana wamepima gogo refu au fupi Ukiona vile Anza kuomba na kuita “Njoo kwa Jina la Yesu” 

5.Kifo cha ghafla.Binadamu ni kama gari jipya hivyo haiwezekani likawa jipya halafu likaharibika bila sababu,hivyo ni lazima augue.Hospitari wanaweza kusema amepata mshtuko wa moyo.Na roho ya kifo huwa inatumwa kwa muda inakaa ndani mwako wala siyo siku moja hivyo jifunze kufuta tarehe ya ya kifo kilichopangwa kwa Jina la Yesu.

6.Mgogoro kwenye familia baada ya msiba.Watu wengine wana macho ya rohoni,moyo unachoongea jua kipo.

7.Maneno ya marehemu wakati anakata roho.Mfano “hao manakuja,hao wananichukua”.Haya maneno yana maana sana,maneno haya yazingatie hivyo ita mtu huyo aliyechukuliwa.

8.Maiti inabadilika sura.Wachawi wanaweza kumchukua mtu na kukuachia kitu.Mara baada ya kugundua kachukuliwa anza kuomba kwa Yesu na tumia maandiko.

9.Watu wanalazimisha kulia.Watu hao waweza kuwa ndugu au watu wengine kama vile majirani.Mfano mfiwa aweza kuambiwa “wewe umefiwa na mama halafu hulii?”.Nia yao ni wewe(mfiwa) ukiri kuwa ndugu yako kafariki.Ukiona hivyo kataa kukiri haraka kuwa mtu waka amekufa.Mfano Yesu alisema Lazaro hajafa bali amelala.Lengo la kulazimisha watu kulia ni kurahisisha mtu kuchukuliwa.mana wasipolia hawawezi kumchukua na kwenda naye.

10.Wanajitokeza watu wanazuia wachungaji(walokole) wasimwombee.Wanaweza kusema hiyo “siyo imani yetu” au “kaombee huko lakini siyo hapa”.

11.Wanandugu wanakataa watu wsiombe wakisema hata akirudi sisi kwetu ni uchuro. 

12.Ndugu wa marehemu wanawaita na kuwapa dawa ili marehemu asije kukutokea tena.

Kwa hiyo ni muhimu inapotokea kuna kifo au tukio limetokea na kuna dalili zilizotajwa, ni vema kuliita Jina la Yesu.

Post a Comment

1 Comments

  1. Kanisa zuri na kufanya kazi ya Mungu kwa ajili ya maendeleo ya umma

    ReplyDelete