MKUTANO
MKUBWA WA INJILI MJINI MOSHI.
Tarehe: 22/10/2013.
Na:
Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima
Somo:
Kafara ya Damu
Lengo la somo hili ni kuwatoa wale waliopo
mapangoni,mashimoni,uvunguni au waliofichwa mahala popote pale kutokana na
kafara ya damu.
Mara nyingi ukisema neno “kafara” watu wanajiuliza
kwamba “kwani huyu ni mganga wa kienyeji?”hii inatokana na watu kutopata
mafundisho kuhusu mambo haya.
Utaona Neno kafara limeandikwa zaidi ya mara
19 kwenye biblia,na ukisoma biblia utaona kuna watu walitoa kafara za damu kwa
ajili ya mafanikio fulani fulani. mfano mfalme wa Moabu ambaye alimtoa mwanae (2wafalme
3:26-27)
Damu
ni nini?
Kumbukumbu
la torati 12:23
Ila ujihadhari kwamba usile damu, kwani ile damu ndiyo uhai; na
uhai usile pamoja na nyama.
Mambo ya Walawi 17:11
Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi
hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu;
kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi.
Mambo ya Walawi 17:14
Kwa maana kuliko huo uhai wa mnyama, hiyo damu yake ni moja na
uhai wake; kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Msile damu ya mnyama wa aina
yo yote; kwa kuwa uhai wa wanyama wote ni katika hiyo damu yake; atakayeila
awaye yote atakatiliwa mbali.
Kwa nini Mungu anazuia kunywa damu?
Mungu anazuia kunywa damu kwa
sababu damu ina uhai.
Mwanzo 4:10
Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia
kutoka katika ardhi.
Katika andiko hili tunajifunza
mambo yafuatayo;
1. Damu ina sauti
2. Damu
inaweza kulia.
3. Mungu
anaweza kusikia kilio cha damu
Pia damu
inao uwezo wa kumfuata mtu mana kuna uhai katika damu,utaiona hii katika;
Mathayo 27:24
Basi Pilato alipoona ya kuwa hafai lo lote, bali ghasia inazidi
tu, akatwaa maji, akanawa mikono yake mbele ya mkutano, akasema, Mimi sina
hatia katika damu ya mtu huyu mwenye haki; yaangalieni haya ninyi wenyewe.
Matendo
ya Mitume 5:28
Akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina
hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta
damu ya mtu yule juu yetu.
AINA ZA DAMU.
A.
Damu inayonena mazuri(mema)
B.
Damu inayonena mabaya.
A.
Damu inayonena mazuri(mema).
Damu ya Yesu ndiyo unayonena mema,Damu ya
Yesu inanena mafanikio,kuinuliwa,ushindi,uwezo na mambo yote mema.
Waebrania 12:24
Na Yesu mjumbe wa agano jipya, na
damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.
B. Damu inayonena mabaya.
Wachawi,waganga wa kienyeji,washirikina nao
wana madhabahu zao. Mfano, wachawi wakitaka kuloga huwa wanakutana mahali, na
kawaida yao huwa wanakutana kwa vikundi, mfano wachawi wa kibosho,wachawi wa
Marangu huwa wanakutana mahali na kumwaga damu,na mahali hapo wanapokutana
ndipo madhabahu yao ambapo kuhani wao wa madhabahu ni Shetani.
Kumbuka damu huwa inamwagwa kwa ajili ya
madhabahu.
Madhabahu
ni nini? Madhabahu ni daraja kutoka ulimwengu wa roho kwenda ulimwengu
wa mwili na kutoka ulimwengu wa mwili kwenda ulimwengu war roho.
Madhabahu huwa inaundwa na vitu vifuatavyo;
1) Madhabahu
yenyewe
2) Kuhani
wa madhabahu
3) Mungu
wa madhabahu
4) Nguvu
za madhabahu
5) Watu
wa madhabahu
Mwanzo
8:20
Nuhu akamjengea Bwana madhabahu; akatwaa katika kila mnyama aliye
safi, na katika kila ndege aliye safi, akavitoa sadaka za kuteketezwa juu ya
madhabahu.
Mwanzo 12:7
Bwana akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye
huko akamjengea madhabahu Bwana aliyemtokea.
Mwanzo 13:4
Napo
ndipo palipokuwa na madhabahu aliyofanya hapo kwanza; naye Abramu akaliitia
jina la Bwana hapo.
Maelfu ya wakazi waliokusanyika katika uwanja wa mashujaa Mjini Moshi siku ya jumanne tarehe 22.10.2013 kwenye mkutano wa Injili, na Mchungaji Kiongozi wa kanisa la Ufufuo na Uzima lenye makao yake makuu Kawe jijini Dar es Salaam.
0 Comments