google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

UJUMBE: VITA NA WALIOKUFA KATIKA DHAMBI

Mch.Kiongozi Josephat Gwajima
Jumapili Tarehe 17.11.2013

Na Mch. Josephat Gwajima


Nimeamua kuliita hili somo vita sababu tunakwenda kupigana vita moja kwa moja na majeshi ya wafu waliokufa katika dhambini


1 Samwel 28:6-20

“…Ukanipandishie yeye nitakaye mtaja kwako…” tunaoana hapa mfalme anakwenda kwa mganga wa kienyeji anaomba apandishiwe mtu aliekufa miaka mingi, Hapa tunaona kumbe mtu aliekufa anaweza kupandishwa na waganga wa kienyeji kutoka kuzimu na akapanda/akazuka.  

1 Samwel 28:11 “…Nipandishie Samwel...” hapa tunaona Samwel alikuwa amekufa lakini mfalme sauli anamwambia mganga wa kienyeji nipandishie Samweli. 
1 Samwel 28:15 “…Ndipo Samwel akapanda na akamwambia mbona umenitaabisha mimi hata kunipandisha juu...”  Kumbe mtu aliekufa anaweza akapandishwa na akazuka kikweli kweli (Samweli akazuka juu),  
1 Samwel 28:19 “….Tena pamoja na wewe Bwana atawatia Israel mikononi mwa Wafilisti; hata na kesho wewe na wanao mtakuwepo pamoja nami…” Haya ni maelezo anayoyatoa Samweli baada ya kuzuka juu. Akatoa maelezo kwamba baada ya siku tatu utakufa wewe na wanao na mtakuwa mahali hapa name, yaani na nyie mtapandishwa kama mlivonipandisha mimi.



Ukisoma theolojia kuna ubishani mwingi unaendelea, wanatheolojia wengi wanasema sababu Samwel alikuwa mtu wa Mungu, sasa ilikuaje mpaka mganga wa kienyeji akaweza kumpandisha, hivyo husema huyu hakuwa Samweli bali ni pepo (Samweli feki). Lakini mimi nataka nikuambie kuwa huyo alikuwa ni Samweli mwenyewe ndio maana aliweza kumpa maelezo mengi sana, ikiwemo kwamba wewe umemuacha Bwana, na umeamua kunitaabisha kunipandisha juu, hivyo baada ya siku tatu wewe na familia yako mtakufa.



Mfalme Sauli alipoona hajibiwi kwa maono wala kwa ndoto, ndio maana akaamua aende kwa mganga wa kienyeji, ndio maana mimi huwa na kwambia kila kiongozi ambaye hajaokoka anamganga wake wa kienyeji, Mwanadamu kwa asili huwezi ukawa mtupu, ni lazima uwe umeungamanika na madhabahu ya mwanakondoo ama madhabahu ya lusifa. Mimi mwenyewe unavyoniona hapa kuna mamlaka nyuma yangu nimeungamanishwa nayo. Usifikiri leo Ufufuo na Uzima tupo hivi, ukadhania tumeibuka buka tu, hapana kuna vita huko nyuma tumepigana.



Sauli amekwenda kwa mganga wa kienyeji akaomba apandishiwe Samweli ili amuulize limpasalo kutenda. Sauli alijificha ili asijulikana na mganga wa kienyeji kama ni mfalme, maana wafalme walikuwa hawaruhusiwi kwenda kwa waganga wa kienyeji. Baada ya mganga wa kienyeji kuanza kumpandisha Samweli alipiga kelele, akamwambia mbona umenidanganya, (mganga wa kienyeji viliumana na samweli alivokuwa anazuka), Sauli akauliza kwanai anayezuka ni nani akamwambia akasema ni mzee anamavazi meupe anazuka katika nchi. Hapo usifikiri kiliwekwa kikopo cha maji, Sauli akamuona Samweli kwenye maji hapana, Samweli alipanda akaanza kuongea ndani ya mganga wa kienyeji. Inanifurahisha hiimaana mganga wa kienyeji badala ya kupandisha vibwengo akapandisha Samweli, na Samweli akatoa maelekezo.

Mchungaji Kiongozi,Josephat Gwajima, akihubiri ndani ya nyumba ya ufufuo na uzima, Kawe, Dar es Salaam


Watu wakifa wanakwenda wapi?



Kabla Yesu hajafa msalabani kuna sehemu ilikuwa inaitwa shiol hili neno ndio hilo limetafsiriwa na biblia linaitwa kuzimu, yaani ulimwengu wa wafu, ama eneo wanalokaa wafu. Waliokufa katika dhambi ama waliokufa katika haki. Shiol ilikuwa imegawanyika sehemu mbili shiol ya watu waliokufa katika haki na shiol ya watu waliokufa katika dhambi, na hii ilikuwa kabla Yesu hajafa msalabani.  
Mwanzo 37:35 “…Nitamshukia mwanangu hata kuzimu nikiwa nasikitika…” Yaani hapa Yakobo anamaanisha akifa atamshukia mwanae Yusufu huko kuzimu, hii ilikuwa ni kuzimu ya waliokufa katika haki.  
Torati 32:22 “…Moto umewashwa kwa hasira yangu unateketea hata chini ya kuzimu…” Hii ni kuzimbu ya waliokufa katika dhambi.

“Kusimu upande wa wenye haki, na kuzimu upande wa waliokufa dhambini Kabla ya Yesu Kristohajafa msalabani”

1 Samweli 2:6 “…Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu…” Zaburi 6:5 “…Maana mautini hapana kumbukumbu lako; katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?...” Zaburi 16:10 “…Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu…” Yuda 1:6 “...Amewaweka vifungo vya milele chini ya giza…” kuzimu kwa lugha ingine ni chini ya giza kwenye vifungo vya milele.

Yesu alipokufa akashuka kuzimu ya waliokufa katika dhambi akamnyang’anya yule joka ufunguo wa kuzimu na mauti, halafu akaeleke upande wakuzimu ya Ibrahimu (kuzimu ya walikufa katika haki) akawaambia yule uzao wa mwanamke ndio mimi, akawahubiria manabii wote huko kuzimu, na kuwaambia nimekuja kuwahamisha twende juu mbinguni, huku sio mahala penu. Yale makaburi kufunguka ilikuwa ni ishara ya uhamisho wa watu wote waliokufa katika haki kutoka kuzimu ya chini na kwenda mbinguni (paradiso) kule Yesu anakaa. Yesu akawaambia sasa tunahama huku tunaenda paradiso. Kwa hiyo baada ya hapo kuzimu ikawa ni mahali pa wafu waliokufa kwatika dhambi na paradiso (mbinguni) ikawa ni makao ya waliokufa katika haki huko wakimuimbia Mungu,na kufurahi.

Sasa kama vile Samweli alivyopandishwa kutoka kuzimu, kaganga kamama kakampandisha Samweli juu, hivyo ndivyo ambavyo leo mtu aliekufa katika dhambi inawezekana akaitwa na waganga wa kienyeji na akaja, wakamtumia kuharibu ukoo kama wawezavyo, Samweli alipanda lakini mganga alishindwa kumpa maelekezo sababu alikuwa mtakatifu akiwa duniani, lakini mababu na mabibi waliokufa katika dhambi wakipandishwa wanaamrishwa wafanye kile mganga anataka.




Kama tulivyoona aliekufa katika haki akaenda mbinguni, humuimbia Mungu na kufurahi huko mbinguni, na wale waliokufa katika dhambi hushuka kuzimu (kifungoni) na kutumika kwa kazi za kuzimu. Na ndio maana leo nasema lazima tupigane nao vita.



Unapokata roho huwa kuna malaika maalumu wanaochukua roho yako, kama ulikuwa unatenda dhambi malaika wa giza wanabeba roho yako wanashusha mpaka kuzimu(gereza la milele), na kama ulikuwa unatenda haki, malaika kutoka mbinguni wanabeba roho yako na kuipeleka mbinguni (pradiso), Ufunuo 20:13. “…Kuzimu ikawatoa watu waliokuwa ndani yake…” Kuzimu ni makao makuu ya shetani, na ziwa la moto ni sehemu ya hukumu ya wale waliokufa katika dhambi, ukishafika hapo unakuwa mfungwa, na unaanza kumtumikia shetani. Babu yako yule aliekufa katika dhambi yupo kuzimu hajakaa tu kule, yupo anapiga mzigo huko, ndio maana utasikia watu tunaowarudisha msukule hapa, ama watu waliokuwa wamekufa wakifufuka hapa kwetu utasikia kazi yangu ilikuwa ni kwenda kwenda kuua watoto wadogo mahosipitali wengine utasikia nilikuwa nasababisha ajali barabarani, hizo ndizo kazi za wafu huko kuzimu.



Mtu anajiuliza hivi watu wanawezaje kumtupia mtu mapepo hata 1000, unauliza huyu ana akiba ya mapepo kiasi gani, kumbe mengine sio mapepo bali ni watu waliokufa wanatumikishwa na shetani, wapo kuzimu lakini wanatumwa kuja duniani, na huwa wanatumwa kwenye koo zao kufanya uharibifu sababu wao wanazijua hizo koo zao vizuri, ni rahisi kushambulia kwa mafanikio makubwa. Kwanza wanafahamu lugha ya ukoo wenu, wanamfahamu baba wa ukoo, wanafahamu madhaifu yenu yote, ndio maana vita yako huwa inakuwa kali kweli. Shetani huwa anawatuma anawaambiakama vile wewe ulivyokuja huku katuletee shangazi yako, ndio maana utasikia watu wanalalamika bibi yangu alikufa kwa kansa na mama yangu nae kwa kansa na mimi nina kansa sasa hivi, huu ni ugonjwa wa ukoo! Hakuna ugonjwa wa ukoo ni wafu wanatenda kazi katika ukoo.

Makundi yanayoshambuliwa sana na majeshi ya wafu

1.      Wale wanaochukua majina ya ndugu wa ukoo ambao hawajaokoka (majina ya mabibi, mababu, shangazi).

Tuangalie sana majina tunayowapa watoto, utasikia mtu anamwita mtoto dragon, astrorogy, au momony angalia utalia, usimpe majina ya ndugu wa ukoo waliokufa watoto wako kama hujui maana yake, chagua majina yanayompa utukufu Mungu, Glory, Ruth, Grace….

Kwanini agano jipya linaanza na kutaja ukoo wa Yesu?

Hii walitaka kutuonesha kwamba ukoo wa Yesu hauna mganga wa kienyeji, wala msoma nyota, wala darweshi, wate walikuwa watu wa haki.

2.      Wale wanaopenda/wanaoendekeza  mila za familia

Utasikia desturi ya ukoo wetu ndugu yeyote anaekufa wote tutanyolewa vipara, mtoto akizaliwa lazima kitovu apewe shangazi, lazima tukajengee makaburi ya babu. Ukiwa unashiriki hizi taratibu lazima majeshi ya wafu yatakupata tu.

3.      Wale wanaopenda makabila kuliko kumpenda Mungu



Namna ya kuomba

Kwa jina la Yesu ninajitenga kabisa, na watu waliokufa kwenye dhambi. Mimi ni wa ukoo wa Yesu, ninajitenga na nyie kwa jina la Yesu. Jina lolote la mtu alielala katika dhambi, ninajitenga nalo kwa jina la Yesu

Jitenge na umasikini wa ukoo, umasikini wa bibi, umasikini wa babu, umasikini wa shangazi, jitenge na ukoo wako kwa damu ya Yesu, najitenga kutoka babu nababu na babu, nawaamuru muachie mali zangu, achia afya yangu, kata kamba zote za ukoo, kamba za familia kwa jina la Yesu.

Post a Comment

0 Comments